June 05, 2014

   

Waziri wa nchi, ofisi ya makamu wa rais (mazingira) Binilith Mahenge.   

Vijana nchini Tanzania wametakiwa kushiriki kikamilifu katika suala la usafi wa mazingira kwa kuwa wao ndio wanauwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko kwa kukataa uchafu katika maeneo wanayoishi.

Wito huo umetolewa leo jijini Dar-es-Salaam na vijana kutoka vikundi mbalimbali ambao wameshiriki kufanya usafi wa mazingira katika maeneo kadhaa ya jiji la Dar-es-Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya mazingira duniani hii leo.
Wakizungumza kwa pamoja Vijana hao Bw. Charles Lupiliani ambaye pia ni afisa wa bodi ya utalii mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Oyite Tungaraja kutoka shirika lisilo la kiserikali la Voice Giving wamesema vijana wana wajibu wa kuhakikisha usafi wa mazingira ni jukumu lao ambalo wanastahili kulipa kipaumbele ili kuepukana na magonjwa.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE