July 04, 2014

 Mrisho-Ngasa-in-on-of-Taifa-Stars-matches
Mrisho-Ngasa-in-on-of-Taifa-Stars-matches      
DURU za habari zinaeleza kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzaniam Taifa stars, Mholanzi, Mart Nooij amemuondoa winga machachari wa timu hiyo na klabu ya Yanga, Mrisho Khalfan Ngassa `Anko` katika kikosi kitakachopepetana na Msumbiji `Black Mambas`.  Imeelezwa kuwa Nooij amefikia maamuzi hayo baada ya Ngassa kushindwa kuripoti katika kikosi chake siku kilipojipima ubavu dhidi ya Botswana na kulala mabao 4-2, mjini Gaborone.  Kabla ya mechi hiyo, kocha Nooij alimuita Ngassa, lakini alikaidi na kwenda Bondeni, Afrika kusini kufanya majaribio na klabu inayoshiriki ligi ya huko, Free State Stars ambako alifuzu, lakini uhamisho umekuwa mgumu.  Ngassa baada ya kufuzu majaribio, klabu ya Free state ilitangaza kutuma ofa ya dola elfu 80 sawa na milioni 130 za Kitanzania, lakini inasemekana Yanga waligoma.  Hata hivyo uongozi wa Yanga kupitia kwa katibu mkuu, Beno Njovu alisema kuwa Free State hawajafika mezani kuzungumza nao bali wanasikia kwenye vyombo vya habari

CHANZO SHAFII DAUDA

Related Posts:

  • Diamond na Rick Ross kuachia Kolabo yao December 1    Msanii wa Bongo Flava, Diamond Platnumz amesema kuwa kolabo yake na rapper Rick Ross itatoka Desemba Mosi mwaka huu. Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Hallelujah’ amesema hayo ka… Read More
  • Official Video: Davido - Fia    Sony Music Entertainment International Limited Wanakuletea wimbo mpya kabisa wa mwanamuziki Davido kutoka nchini Nigeria.Enjoy sasa kwa kuutazama hapa chini        &nbs… Read More
  • M2 The P kurudi kivingine, Jodan na Mirror wapo pia   Msanii wa muziki Bongo M2 The P ametangaza kurudi kivingine katika game pamoja na Mirror na Jodan. Mirror na Jodan ambaye walikuwa chini ya usimamizi wa Marehemu Ngwea wamekuwa kimya kwa muda sasa, hata hivyo … Read More
  • Hawa ndiyo wanaomkwamisha Baraka The Prince Msanii Baraka The Prince amemlaumu meneja wake wa zamani chini ya RockStar 4000 Seven Mosha pamoja na mpiga picha maarufu Mx Carter, kuwa ndio wanaohusika na kufelisha kazi yake mpya YouTube. Baraka ameyasema hayo a… Read More
  • Mambo makubwa manne kutoka ACT Wazalendo leo   Chama cha ACT Wazalendo kimeeleza mambo manne kuhusu kupekuliwa kwa  Ofisi za chama hicho na Jeshi la Polisi. Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi, Ado Shaibu imeeleza mambo ha… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE