October 27, 2014



Askari polisi wawili wa kituo cha polisi cha wilaya ya Geita, wamelazwa katika hospitali ya wilaya hiyo baada ya kujeruhiwa kwa risasi wakati wa mapambano ya kujibizana na majambazi sita kuzuia uhalifu uliopangwa kufanyika katika kijiji cha Nyakagwe wilayani humo.

Waliojeruhiwa ni Koplo E.18O9 Said na Konstebo G.6212 Hamisi wote wa kitengo cha upelelezi huku jambazi mmoja anayedaiwa ni raia wa Burundi akiuliwa na wananchi baada ya kujeruhiwa kwa risasi na polisi kisha kuchomwa moto baada ya kugundulika amejificha kichakani.

Tukio hilo lililotokea juzi usiku huku mganga wa zamu wa Hospitali ya Wilaya ya Geita, Dk. George Rweyemera, akisema aliwapokea majeruhi hao na hali zao zinaendelea vizuri. Hamis alijeruhiwa risasi ya mguu wa kulia na Said mkono wa kushoto.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nyakagwe, Simon Kazungu, alisema wananchi walilipongeza Jeshi la Polisi na askari hao kupambana na majambazi hao na kuzuia uhalifu uliopangwa kutendeka.

Kazungu alisema polisi hao walipelekwa katika kijiji hicho kuongeza nguvu baada ya kuwapo taarifa za kutokea tukio la ujambazi usiku huo na ghafla walivamiwa na kumiminiwa risasi zilizowajeruhiwa kabla ya kujibua mapigo kwa dakika 20 na majambazi kuzidiwa nguvu.

Majambazi hao baada ya kutoroka wawili kati yao wakiwa na bunduki aina ya SMG, walisakwa na wananchi baada ya kuifuata damu iliyokuwa ikimtoka mwenzao na kumkuta akiwa amejibanza na kuanza kushambuliwa hadi kufa kisha kuteketezwa kwa moto.

Kazungu aliongeza kuwa baada ya kumpekua walimkuta na nyaraka zilizomtambulisha ni raia wa Burundi.

Wiki iliyopita watu wengine wenye silaha walivamia kijiji hicho maarufu kwa shughuli za uchimbaji madini ya dhahabu na kuiba kiasi Sh.300,000.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Joseph Konyo, alithibitisha kutokea  tukio hilo.

Related Posts:

  • official video: Sio Kama Wao - Agatha ft Joh Mkristo Kwa mara ingine tena Mwanamuziki toka mkoani Morogoro anaitwa Agatha Mbale, anadondosha ngoma yake mpya inaitwa Siyo kama wao. Agatha ameshusha hii baada ya ngoma zake za Shujaa na Mawenge kufanya poa . Tazama hapa c… Read More
  • Mbunge wa Kilosa atoa msaada wa Kisima na Mabati kwa wananchi wake  Wakazi wa Kata ya Rudewa wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro wakiwa makini kumsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo Mbraraka  Ba Waziri wakati alipokua akifanya mkutano na wananchi hao akiskiliza kero na kutoa utatuzi… Read More
  • AC Milan Yafungiwa WAKON G­WE wasokanchini Italia, AC Milan wamefungiwa ku­shiriki michuano ya Ulaya kwa mwaka mmoja kuto­kana na kukiuka kanuni za soka. Timu hiyo ilikuwa iki­jiandaa kushiriki katika mi­chuano ya Europa League msimu u… Read More
  • Official Video: Sihitaji - Strevol Kutoka mji kasoro Bahari Morogoro, maeneo ya Forest ndani ya studio za Kwanza Record chini ya mtayarishaji Vennt Skillz, Mokomoko Movemennt inamdondosha kwenu na kumtambulisha rasmi zao lingine kabisa chini ya Lebo hiy… Read More
  • CUF yajitoa rasmi, waipa nasaa UKAWA Chama cha wananchi CUF, Kimetangaza rasmi kujitoa katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa marudio unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao nchini. Akitoa taarifa kwa umma Naibu Mkurugenzi wa Habari , Uenezi na Mahusiano ya Umma wa… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE