January 03, 2015


. 
Stori ambayo imechukua nafasi kubwa ya kujadiliwa kuanzia mida ya jioni ya jana  Dar es salaam ni kuhusu kikundi cha wezi wanaotumia ubabe maarufu kama Panya Road ambacho kinaaminika kuvamia maeneo kadhaa ya Dar es Salaam ikiwemo Sinza, Mwananyamala, Tabata na sehemu nyingine.
Taarifa ambazo zilianza kusambaa kutoka kwa mashuhuda ni kwamba Wezi hawa walikua wakipiga watu, kupora vitu mbalimbali na hata kuharibu baadhi ya magari na pikipiki kwa kuvunja taa wakati wakipita kwenye mitaa mbalimbali.
Baada ya taarifa kusambaa Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova alizungumza kwenye TBC1 na kusema hawezi kupinga uhalifu kufanyika leo mtaani lakini sio kwa kiasi hicho ambavyo imeripotiwa, yaani habari imekuzwa kuliko ukweli wenyewe.
Miongoni mwa  aliekumbwa na huu mkasa ni mtangazaji wa Clouds FM Efphraim Kibonde kama ambavyo  anasikika akizungumza kwenye hii sauti hapa chini.Pia mtayarishaji wa muziki wa Bongo freva Sheddy naye amekumbwa na mkasa huu

SAUTI YA KIBONDE


PRODUCER SHEDDY

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE