January 19, 2015

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/5e392c4d9cc51aa660a90bec0219f5d3_XL.jpg 
 Wanamapinduzi wa Kishia wa Ansarullah wa nchini Yemen wamepigana na vikosi vya serikali huko Sana'a mji mkuu wa nchi hiyo. Watu walioshuhudia wamesema kuwa, sauti za risasi na milipuko kadhaa zimesikika huko Sana'a na karibu na ikulu ya Rais kusini mwa mji mkuu huo. Maafisa usalama wa Yemen walifunga barabara zinazoelekea katika ikulu ya rais, huku ripoti nyingine zikisema kuwa mapigano yamejiri ndani ya ikulu hiyo, huku moshi ukishuhudiwa katika eneo hilo.
Wakati huo huo kanali ya televisheni ya wapiganaji wa Kihouthi imetangaza kuwa vikosi vya jeshi la Yemen vilifyatua risasi wakati vikipiga doria katika ikulu ya rais, hatua iliyosababisha ghasia. Mivutano imekuwa ikishadidi huko Yemen kati ya wapiganaji wa Ansarullah wanaojulikana pia kwa jina la Mahouthi na vikosi vya serikali, baada ya wapiganaji hao wa Kishia kumtia mbaroni Ahmed Awad bin Mubarak, mkurugenzi wa ofisi ya Rais Abdrabuh Mansour Hadi wa Yemen. Mubarak alitiwa nguvuni katika kituo kimoja cha upekuzi katika mkoa wa Hada kusini mwa Yemen.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE