Polisi wawili wameuawa katika machafuko yanayoendelea nchini Burundi
katika mwendelezo wa maandamano ya wapinzani ya kupinga hatua ya Rais wa
nchi hiyo Pierre Nkurunziza ya kuamua kugombea katika uchaguzi mkuu
ujao nchini humo. Polisi ya Burundi imetangaza kuwa, mbali na polisi hao
wawili, mtu mmoja mwengine alipoteza maisha katika shambulio hilo
lililotokea jana usiku jijini Bujumbura. Kwa mujibu wa mashuhuda,
shambulio hilo lilitokea majira ya saa moja na nusu usiku katika eneo la
Kamenge, kaskazini mashariki mwa mji huo. Maandamano ya kupinga uamuzi
wa Rais Nkurunziza kutaka kugombea katika uchaguzi wa rais ujao,
yamezorotesha uchumi wa nchi hiyo. Hayo yanajiri katika hali ambayo rais
huyo ameendelea kushikilia msimamo wake wa kugombea kwenye uchaguzi
huo. Akihutubia sherehe za Mei Mosi hapo jana, Rais huyo kijana, mbali
na kukosoa maandamano ya wapinzani aliwataja watu wanaoandamana kuwa ni
watoto wadogo wanaojiingiza katika mambo yasiyowahusu.
JACKLINE ISARO AANZA RASMI MAJUKUMU KUTUMIKIA NGOKOLO...."SITAKUWA DIWANI
WA MANENO"
-
Diwani wa Kata ya Ngokolo, Jackline Isaro, ameanza rasmi majukumu yake
baada ya kula kiapo cha udiwani leo Desemba 4, 2025, akiahidi kusimama
imara katika...
2 hours ago





0 MAONI YAKO:
Post a Comment