May 13, 2015

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza 
 Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza

Meja Jenerali wa Burundi Godefroid Niyombire alisema siku ya Jumatano kuwa alikuwa anafanya kazi na makundi ya vyama vya jamii, viongozi wa dini na wanasiasa kuunda serikali ya mpito, baada ya yeye na maafisa wa juu kumtimua rais.
Niyombare, ambaye alisema Rais Pierre Nkurunziza alikiuka katba kwa kutaka kugombea muhula wa tatu, alitoa maoni hayo kwa waandishi wa habari kwenye kambi ya jeshi. Baadae kauli hizo zilitangazwa kwenye vituo vya redio nchini humo.
  
Kiongozi wa Mapinduzi  Meja Jenerali Godefroid Niyombare
18:55 Mwandishi wa BBC aliyeko Dar es Salaam anasema kuwa ndege ya rais Nkurunzinza imepaa ikielekea Bujumbura
 
 18:53 Kiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza kufungwa kwa mipaka
18:45 Mwandishi wa BBC huko Bujumbura Kazungu Lozy anasema watu wangali wanasheherekea
18:40 Rais Nkurunzinza ameingia ndani ya gari lake na kuondoka mjini Dar es Salaam akionesha dalili kuwa yuaelekea Burundi


18:37 Kiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid Niyombare ameamrisha wanajeshi kuzuia rais Nkurunzinza kutua Burundi
18:30 Rais Pierre Nkurunziza anatarajiwa kuhutubia taifa baada ya kurejea kutoka Tanzania amesema msemaji wake Willy Nyamitwe.

  
Wananchi waendelea kusheherekea Bujumbura kufuatia tangazo la ''Mapinduzi'' 

8:25 Generali Niyombareh ametoa amri kwa majeshi kuungana na kulinda viwanja vya ndege kote nchini humo
18:20 Generali aliyeongoza ''Mapinduzi'' leo asubuhi amewataka maafisa wa jeshi na polisi kufanya kazi kwa pamoja ilikulinda usalama wa nchi hiyo.

Rais kikwete alipohutubia waandishi wa habari Dar es Salaam akiandamana na Rais Nkurunzinza

18:15 Viongozi wa kanda ya Afrika wametaka makundi hasimu kutulia na kukubali hali ya kikatiba Kurejea
18:10 Esipisu amesema kuwa rais Uhuru Kenyatta anaunga mkono kurejeshwa kwa utawala wa kikatiba


 
 Maafisa wa jeshi la Burundi wakisheherekea Barabarani Bujumbura 
 18:07 Msemaji wa rais wa Kenya Manoah Esipisu amesema kuwa viongozi wanataka hali ya kawaida irejee huko Burundi
 8:06 Rais wa Tanzania amekashifu ''mapinduzi'' yaliyotoke leo huko Burundi
18:05 Rais amesema hayo katika mkutano wa upatanishi wa viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki
18:01 Ujumbe wa mtandao wa facebook wa urais nchini Burundi umekanusha kutokea kwa ''Mapinduzi''.
 8:01 Viongozi hao wanakutana dar es salaam kujaribu kutatua mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Burundi
18:01 Rais Jakaya Kikwete amesema hayo katika mkutano wa upatanishi wa viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki
18:00 Rais wa Tanzania amekashifu ''mapinduzi'' yaliyotoke leo huko Burundi
17:55 Msemaji wa rais Nkurunzinza ameiambia BBC kuwa asilimia 95 ya taifa hilo ingali salama na wala hakuna tashwishi.
 7:50 Manuari zaidi zaonekana barabarani mjini Bujumbura
17:45 Ujumbe wa mtandao wa facebook wa urais nchini Burundi umekanusha kutokea kwa ''Mapinduzi''.
17:30 Msemaji wa rais Nkurunziza,Willy Nyamitwe ameiambia BBC kuwa rais huyo angali madarakani na kuwa hajaondolewa madarakani
 
 zaidi ingia bbc.com

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE