July 19, 2015


Bernard Membe ajiuzulu siasa nchini Tanzania
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje nchini, Bernard Membe, amesema hatogombea wadhifa wowote kwenye uchaguzi mkuu ujao na kwamba anapanga kujishughulisha na masuala yake ya kibinafsi.
Membe ambaye alikuwa akitafuta tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuwania urais mwezi Oktoba lakini akashindwa kufikia lengo hilo, amesema kuwa, hatotafuta nafasi ya ubunge katika jimbo lake la Mtama. Hata hivyo amesema ataendelea kukiunga mkono chama chake cha CCM na atampigia debe mgombea urais aliyeteuliwa na chama hicho, Bw. John Magufuli.
Awali kulikuwa na tetesi kwamba Membe angegombea ubunge baada ya kukosa nafasi ya kuwania urais kwa tiketi ya CCM.
Huku hayo yakijiri, chama tawala nchini CCM kinaendelea kupata pigo baada ya baadhi ya wabunge wake kutangaza kuwa hawatogombea tena nafasi zao kupitia chama hicho kwenye uchaguzi mkuu ujao. Mbunge wa Kahama, James Lembeli ni mwanachama wa CCM wa hivi karibuni kutangaza kuwa hatatetea kiti chake kupitia chama hicho kwenye uchaguzi wa Oktoba mwaka huu. Tayari madiwani 20 wa CCM katika jimbo la Monduli wametangaza kuhamia Chadema na kumtaka mbunge wao, Edward Lowassa kufuata mkondo huo.

Related Posts:

  • Rais aondoa marufuku ya nyweleMarufuku hiyo ilikuwa imetolewa mapema mwezi huu Rais wa Gambia Yahya Jammeh ameondoa agizo la kuwataka wafanyakazi wa kike serikalini wawe wakijifunika nywele wakiwa kazini. Marufuku hiyo, iliyotolewa tarehe 4 Januari, … Read More
  • Watu weusi waachwa nje tuzo za Oscars   Filamu ya The Revenant inaongoza kwa kushindania tuzo vitengo vingi     Waigizaji na waelekezi wa filamu watakaopigania tuzo kuu za sanaa duniani za Oscar wametangazwa na kwa mwaka wa pili haku… Read More
  • Tumekuwekea hapa Magazeti ya leo hii upitie japo kwa ufupi tu Habari ndugu yetu mpendwa. Karibu katika magazeti yetu ya leo hii Ijumaa January 15 2016 upitie japo kwa ufupi tu kile kilichopewa kipaumbele leo hii. Share na mwenzio … Read More
  • Tanzia: Celine Dion afiwa na mumewe Rene Angelil alihudumu kama meneja wa Celine Dion hadi 2014 Rene Angelil, mume wa mwanamuziki mashuhuri duniani Celine Dion, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 73, mwanamuziki huyo ametangaza. Bw Angelil, aliyemuoa Dion … Read More
  • Tazama matokeo ya kidato cha pili hapa     Matokeo ya kidato cha pili 2015 yametoka. Ubalozini.blogspot.com tunakuletea kwa ukaribu zaidi matokeo hayo hapa,   Bofya hapa kupata matokeo ya kidato cha pili 2015 … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE