Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (PTA),
Awadh Massawe akizungumza na wanahabari wakati akikabidhi hundi ya
sh.milioni mbili kwa Taasisi ya Habari Development Association Dar es
Salaam jana asubuhi.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (PTA),
Awadh Massawe (kushoto), akikabidhi mfano wa hundi ya sh.milioni mbili
kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Habari Development Association (HDA), Kunze
Mswanyama (kulia), Dar es Salaam jana asubuhi kwa ajili ya kuandaa
mafunzo ya kuwawezesha waandishi wa habari kujenga weledi wa kufanya
tafiti na kuandika habari za kupambana na ujangili. Wa pili kushoto ni
Ofisa Mwandamizi wa Mawasiliano wa TPA, Focus Mauki na Katibu Mkuu wa
Taasisi hiyo, Benard James.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Habari Development Association (HDA), Kunze Mswanyama
(kulia), akizungumzia kuhusu mafunzo na umuhimu wa wanahabari katika
kupambana na ujangili wa rasilimali za taifa kabla ya kukabidhiwa msaada
wa sh.milioni 2 kutoka PTA. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa PTA, Awadh
Massawe.
Kaimu Mkurugenzi wa PTA, Awadhi Massawe (katikati), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana. Kushoto ni Ofisa Mwandamizi wa Mawasiliano wa TPA, Focus Mauki na Mkurugenzi wa Taasisi ya Habari Development Association (HDA), Kunze Mswanyama.
Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA
ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imetoa sh. milioni 2 kwa
Taasisi ya Habari Development Association kwa ajili kuandaa mafunzo ya
kuwawezesha waandishi wa habari kujenga weledi wa kufanya tafiti na
kuandika habari za kupambana na ujangili.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Awadh Massawe alikabidhi hundi ya thamani ya
fedha hizo kwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Kunze Mswanyama jijini Dar es
Salaam jana.“Tunaunga mkono juhudi hizi za kupambana na ujangili,”
alisema Massawe.
Alisema
TPA imefanya hivyo kwa kuwa nchi ina tatizo la uwindaji haramu hasa wa
ndovu na usafirishaji wa pembe za ndovu na kulisababishia hasara taifa
kupitia mipaka yake.
Alifafanua
kuwa bandari ya Dar es Salaam ni sehemu ya mpaka wa taifa, hivyo lazima
TPA iunge mkono juhudi za kuelimisha jamii na kuzuia uhalifu huo.
Massawe
alisema kwa sasa wanatarajia kufunga kamera 400 za CCTV ili kuimarisha
ulinzi na kuwa skana tatu zimeletwa bandarini kwa ajili yakuziongezea
nguvu skana mbili zilizopo.
Pia,
alisema wanatarajia kupata msaada wa mbwa maalumu wa ulinzi
watakaotolewa na Serikali ya Marekani. Alisema TPA inaendelea kuwajengea
uwezo wafanyakazi kimaadili ili kuendelea kufanya kazi kwa weledi na
uaminifu kwa faida ya taifa.
Mkurugenzi
wa taasisi hiyo, Mswanyama alisema fedha walizopewa watazitumia kwa
kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari 54 kwa masuala ya ujangili kupata
weledi na kutafiti na kufichua ujangili. “Tunahitaji kujenga uwezo wa
kupambana na ujangili ili taifa liweze kunufaika nazo,” alisema.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment