Mgombea huyo wa ACT Wazalendo Khamis Iddi Lilla ametoa ahadi hiyo
alipokuwa akinadi sera katika viwanja vya Kiembesamaki ambapo amesema
chama cha ACT kinawajua waletaji hao wa madawa ya kulevya na serikali
yake itaunda kikosi cha kisasa chenye vitendea kazi vyote
vianavyohitajika.
Akizungumzia utendaji wa serikali katika kushugulikia sekta za
kijamii mgombea huyo amesema kazi ya kwanza akiingia madarakani itakuwa
ni suala la kutoa elimu kwa watoto hadi wazee na afya hospitali na vituo
vyote kuwa na madawa na madaktari.
Naye mgombea mwenza wa rais wa muungano wa ACT Wazalendo Hamad
Mussa akitafuta kura aliwataka wazanzibari wabadilike na kuacha
kukumbatia vyama vya CCM na CUF.
Kutokana na siku kuu ya Iddi el haj karibu vyama vyote
vimesimamisha kampeni zao hadi kuanzia jumatatu ambapo chama cha NRA
kitafanya mkutano wake wa kwanza huku CCM, CUF, ACT Wazalendo na ADC na
vyama vyingine vikiendelea na kusaka urais wa Zanzibar.





0 MAONI YAKO:
Post a Comment