December 17, 2015

Mourinho
Mourinho alikuwa tayari amekiri Chelsea hawawezi kumaliza katika nne bora ligini
Meneja wa klabu ya Chelsea ya Uingereza amefutwa kazi baada ya klabu hiyo kuandikisha msururu wa matokeo mabaya.
The Blues walishinda Ligi ya Premia msimu uliopita lakini msimu huu mambo yamekuwa kinyume, na wamo nafasi moja tu juu ya eneo la kushushwa daraja ligini.
Bodi ya klabu hiyo ilikutana jana kujadili hatima ya Mourinho chini ya mmiliki wa klabu hiyo, Mrusi Roman Abramovich.
  • Bodi ya Chelsea yamjadili Mourinho
  • Guardiola kuweka wazi hatima
  • Mourinho: Naona aibu
Mreno huyo mwenye umri wa miaka 52 amekuwa Chelsea kwa kipindi cha pili, kilichoanza Juni 2013.
Chelsea walimaliza alama nane mbele kileleni msimu uliopita na kutwaa taji pamoja na Kombe la Ligi lakini mwaka huu wameanza vibaya, wakishindwa mechi tisa kati ya 16 ligini kufikia sasa.
mechi ya mwisho kwa Mourinho kwenye usukani ilikuwa Jumatatu walipochapwa na viongozi wa ligi Leicester City 2-1.
Pep Guardiola, Guus Hiddink, Brendan Rodgers na Juande Ramos na miongoni mwa wanaopigiwa upatu kumrithi

Kwa hisani ya BBC

Related Posts:

  • Tanzania kukumbwa na ukame   Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk.Agnes Kijazi (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam.  Mamlaka ya Hali ya H… Read More
  • Mwizi wa wasanii Clouds huyu hapa   Huyu kijana kushoto amekamatwa kwa kosa la kutapeli watu mbalimbali kwa kutumia majina ya wafanyakazi wa Clouds akiwemo Ruge Mutahaba na kujifanya yeye ndio kiongozi wa idara ya muziki ya Clouds fm na kuwatapeli… Read More
  • Watu 35 wafa kwa mafuriko   Zaidi ya watu 35 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 55 wamejeruhiwa baada ya nyumba zao kuwaangukia na kuwafunika usiku wa kuamkia leo kutokana na mvua kubwa iliyonyesha wilayani Kahama, mkoani Shinyanga  … Read More
  • Wanne wahukumiwa kifo MwanzaMahakama kuu ya Tanzania Mwanza imewahukumu adhabu ya kunyongwa hadi kufa washtakiwa wanne akiwemo mume wa marehemu baada ya kupatikana na hatia ya kumuua zawadi Mangidu [22] wa kijiji cha Nyamalulu kata ya Kaseme wilayani Ge… Read More
  • Bajeti ya jeshi yaboreshwa China    China inasema kuwa bajeti yake ya ulinzi itaongezeka kwa asilimia kumi mwaka huu. Wanajeshi wake wanatarajiwa kupewa dola bilioni 145 na kuendelea na mfumo wa kuongeza bajeti ya jeshi ulioanza miaka 20 iliyo… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE