December 19, 2015

Screen Shot 2015-12-19 at 5.12.22 PM

Hospitali ya Temeke ya jijini Dar es salaam imekusanya zaidi ya Unit 100 za damu zilizotolewa na waumini wa dini ya Kiislamu kutoka Taasisi ya Jamiiyat-Akhlaaqu- Islamiya wakiongozwa na viongozi wa halmashauri ya Manispaa ya Temeke ili kukabiliana na Upungufu wa damu katika hospitali hiyo.
Waumini hao wake kwa waume zaidi ya 150 walianza zoezi hilo la kujitolea damu ikiwa ni muitikio wa kukabiliana na Upungufu wa damu katika hospitali hiyo ambayo ilikuwa na Upungufu wa asilimia hamsini kutokana na wagonjwa wengi kuhitaji huduma ya kuongezewa damu ikiwemo akinamama wajawazito, watoto pamoja na majeruhi wa ajali.
Wakizungumzia zoezi hilo baadhi ya waumini waliojitolea damu wamesema hatua hiyo inaonyesha uzalendo na kuwataka wananchi wengine kujitolea damu ili kuwasaidia wananchi wengine wenye Shida

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE