February 04, 2016

                   
   Familia ya Abdul Bajandar ilishindwa kugharimia matibabu yake

Serikali ya Bangladesh imesema itagharimia upasuaji wa kumtibu mwanamume ambaye anaugua ugonjwa unaofanya mtu kupata dutu zinazofanana na mizizi ya mti mwilini.

Waziri wa afya wa Bangladesh Mohammad Nasim alitangaza hilo baada ya kumtembelea Abul Bajandar, hospitalini Alhamisi.

Bw Bajandar anaugua ugonjwa ambao kisayansi unajulikana kama epidermodysplasia verruciformi.

Ni ugonjwa wa kinasaba ambao humfanya mtu kuota vidutu kwenye ngozi. Hujulikana sana kama “ugonjwa wa binadamu mti”.

Alianza kuota vidutu miaka 10 iliyopita.

“Awali, nilidhani hazina madhara,” Bw Bajandar ameambia AFP.


AFP

"Sasa zimeongezeka na nyingine zina urefu wa inchi mbili hadi tatu katika mikono yangu miwili. Kuna nyingine miguuni,” amesema.

Bw Bajandar alisafiri India kutafuta matibabu lakini familia yake haingemudu gharama.

Sampuli za damu yake na ngozi zitapelekwa kwenye maabara moja Marekani kuchunguzwa zaidi, profesa Abdul Kalam, ambaye ni mtaalamu wa upasuaji wa ngozi ameambia BBC.

Atatibiwa nchini Bangladesh baada ya matokeo ya uchunguzi kutolewa.

Bw Bajandar ni mmoja wa watu watatu wanaougua “ugonjwa wa binadamu mti” duniani, mkurugenzi wa hospitali ya chuo cha Dhaka, Samanta Lal Sen ameambia AFP.

Ni mara ya kwanza kwetu kupata kisa kama hicho hapa Bangladesh.


Source:BBC

Related Posts:

  • TAZAMA NMB ILIVYOSAIDIA KITUO CHA WALIMU TEMEKE   Benki ya Nmb imesaidia kituo cha walimu Temeke Meneja wa kanda ya Dar es salaam ambayo imekabidhi kompyuta mbili na mashine ya kuchapia karatasi(printer) kwenye kituo cha cha walimu wilaya ya Temeke Dar es salaam… Read More
  • TB JOSHUA: UTABIRI WAKE WATIMIA Prophet TB Joshua alitabiri mwaka jana kwamba Nigeria itakua ya kwanza kiuchumi kushinda nchi zote za Africa. Wakati anatabiri. ..nilikua nikiangalia nchi ya Africa Kusini, Misri etc.....niliwaza sana. Jana Imetangazwa kuw… Read More
  • JUMA NATURE ASEMA JOKATE MWEGELO AMEMUIGA Chelewa chelewa, utakuta mwana sio wako!! Ndicho kilichotokea kwa Juma Nature ambaye wazo lake la kuanzisha ndala liliendelea kuwa la mdomoni na ‘kutalk the talk’ ilhali Jokate Mwegelo akileta action kweli kwa ‘kuwalk t… Read More
  • MVUA MOROGORO ZAIDI YA MASAA 24, ZALETA ATHALI KWA WANANCHI Wananachi wa kata ya Mwembesongo wakitemebe kwenye maji baada ya barabara ya kichangani kujaa maji wakitoa maji yaliyojaa dukani kwao  Bi,Hasma Ndehele ambaye ni Kigogo wa CCM kata ya Mji Mpya ak… Read More
  •   Mshambuliaji Emmanuel Okwi. Na Shakoor Jongo FILAMU ya Emmanuel Okwi na timu yake ya Yanga inaendelea, sasa ni ukurasa mpya baada ya mchezaji huyo raia wa Uganda kutoa kauli. Okw… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE