Mtu mmoja ambaye hatukuweza kulipata jina lake mkazi wa Mkamba Kilombero, amekutwa polini akiwa amekatwa miguu yake yote miwili na kutelekezwa polini. Tukio hilo limetokea siku ya juzi katika kata ya Ruaha wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro.Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi kinasema, baada ya bwana huyo kuokotwa akiwa hana miguu, lakini siku ya leo Marc 31 miguu hiyo imeonekana sehemu nyingine jilani na kanisa la ROMA huko huko Ruaha Kilombero. Watu waliomuokota mtu huyo, wanasema mwanzoni walipomuokota, alikuwa akipumua kwa shida sana na baadaye akapoteza fahamu na kumuwahisha katika Hospitali ya Illovo ambapo ndipo alipolazwa mpaka sasa akiendelea kupatiwa matibabu huku jeshi la polisi likiendelea na uchunguzi ili kuwapa wahusika wa tukio hilo.
Sanlam Insurance kutumia Mbio za NBC Dodoma Marathon kufikisha elimu ya Bima
-
KAMPUNI ya Bima ya Sanlam Insurance, mmoja wa wadhamini muhimu mbio za
NBC Dodoma...
24 minutes ago
Ubinadamu now umemwisha mmmh.........
ReplyDelete