March 18, 2016

                      

Raia kumi wa Kenya wameituhumu Serikali ya Tanzania, kwa kukamatwa kwa kuwateka jijini Maputo nchini Msumbiji Januari 2006, ambako walikuwa wakiishi kihalali wakitafuta fursa za biashara, na kisha kuwapakiza kwenye ndege ya kijeshi na kuwaleta nchini Tanzania kwa nguvu.

Kwa upande wake, serikali ya Tanzania kupitia mawakili wake imepinga madai hayo na kuitaka mahakama ya Afrika kutupilia mbali maombi ya watuhumiwa. Tanzania inasema watuhumiwa hao walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere baada ya kuletwa kupitia ndege ya jeshi la Msumbiji.

Wakenya hao wanahoji kuwa kesi yao nchini Tanzania imechukua muda mrefu kwa kuahirishwa mara kwa mara bila sababu. Aidha wanadai kuwa kesi imeendeshwa bila wao kuwa na mawakili wa kuwatetea.

Mawakili wa serikali ya Tanzania pia waliieleza Mahakama ya Afrika kuwa, wawili kati ya raia hao wa Kenya waliofariki wakiwa magereza, walikufa kwa kifo cha kawaida, na kesi iliahirishwa mara kwa mara kutokana na mawakili wa walalamishi kukosa kufika mahakamani siku za kesi.

Wakenya hao walikamatwa miaka kumi iliyopita na kuhukumia kufungwa miaka thelathini jela, baada ya kukutwa na hatia ya kosa la mauaji na ujambazi wa kutumia silaha lililofanyika katika benki ya NMB Tawi la Moshi, mwezi May,2004.

Mahakama ya Africa kuhusu haki za binadamu na za watu iliundwa mwaka 2006 na kuanza kazi zake rasmi mwaka mmoja baadae. Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi februari 2016, Mahakama imepokea kesi 74, ambapo 25 kati ya hizo zimekwisha shughulikiwa, huku kesi 4 zikipelekwa katika Tume ya Afrika ya Watu na Haki za Binadamu nchini Gambia.

Related Posts:

  • Mkurugenzi TPA asimamishwa kazi Waziri wa Usafirishaji Samweli Sitta.  Taarigfa zilizotufiki punde zinasema kuwa Waziri wa Uchukuzi Samuel Sitta amsimamisha kazi kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya Bandari Tanzania mhandisi Madeni Kipande kutok… Read More
  • Runinga zilizojizima kupigwa fainiMamlaka ya mawasiliano nchini Kenya sasa inasema kuwa itavipiga faini vituo vya uninga vya NTV,KTN,Citizen na QTV nchini Kenya kwa kuzima matangazo yao kufuatia hatua ya serikali kuhamia katika matangazo ya dijitali. Mkurugen… Read More
  • Bodaboda wezi wa simu, wakamatwa na kuchomewa pikipiki   Maeneo karibu na Ocean Road, vijana maarufu kwa ukwapuaji wa simu za mkononi wakiwa kwenye pikipiki walimkwapulia dada mmoja simu. tukio hilo lilionwa na mtu aliyekuwa kwenye gari ndipo alipoanza kuwafukuzia na k… Read More
  • CUF- Wampeleka Lipumba UKAWACUF kimesema kimepanga kulipeleka jina la Profesa Ibrahimu Lipumba ili kuomba ridhaa ya kugombea kiti cha urais. Naibu mkurugenzi wa uchaguzi wa chama cha wananchi CUF Bwana Shaweji Mketo amesema chama cha wananchi CUF kimepa… Read More
  • Waliowajeruhi polisi Tanga wasakwaJeshi la Polisi nchini  limesema wanawasaka watuhumiwa waliowajeruhi askari sita kwa risasi mkoani Tanga. Askari hao walijeruhiwa wakati wakifanya kazi ya kuwatafuta watuhumiwa wa uhalifu wa kutumia silaha wanaodaiwa kuw… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE