March 11, 2016


Waislamu Marekani wakosoa chuki ya Warepublican
Waislamu nchini Marekani, wamesema kuwa maneno ya chuki dhidi ya dini tukufu ya Kiislamu yanayotolewa na viongozi wa chama cha Republican, ndiyo sababu ya kuongezeka hujuma na mashambulizi dhidi ya Waislamu nchini humo.
Taarifa iliyotolewa jana na viongozi wa jumuiya za Waislamu nchini Marekani mbele ya waandishi wa habari mjini Washington imemtaka Donal Trump, anayewania kuteuliwa na chama cha Republican kugombea urais nchini Marekani, kuwaomba radhi Waislamu kutokana na matamshi yake ya hivi karibuni yaliyojaa chuki dhidi yao. Itakumbukwa kuwa Jumatano usiku wakati akizungumza na kanali ya televisheni ya CNN, Trump alisema kuwa Uislamu unachafua sura ya Marekani. Nihad Awad, Mkurugenzi wa Baraza la Mahusiano la Kiislamu nchini Marekani amesema kuwa, Trump lazima awaombe radhi Waislamu ambao baadhi yao wanahudumu jeshini, kama ambavyo pia kuna madaktari Waislamu wanaookoa maisha ya mamilioni ya Wamarekani na pia kuna maafisa wa ngazi tofauti serikalini wanaowahudumia raia. Aidha amesisitiza kuwa, mgombea huyo wa nafasi ya urais kwa tiketi ya chama cha Republican anatakiwa kuwaomba radhi wanawake Waislamu ambao kutokana na kuvaa kwao vazi la Kiislamu la hijabu, wananyanyasika na kutengwa katika idara za serikali na mashuleni nchini Marekani. Kabla ya hapo pia jumuiya za Kiislamu nchini Marekani zilikuwa zimetahadharisha kwamba, matamshi ya kichochezi ya Donald Trump, yanawaweka hatarini Waislamu nchini humo.

Related Posts:

  • NECTA: Watakaofanya udanganyifu wa aina yoyote kukiona cha moto Na Said Mwishehe,Blog ya jamii BARAZA la Mitihani la Tanzania(Necta) limetoa onyo kali kwa wamiliki wa shule,walimu na wananchi kutojihusisha na vitendo vya udanganyifu wa mitihani ya Kidato cha Sita na Koz… Read More
  • Yanga yamlilia Chamangwana   Timu ya soka ya Yanga ya jiji Dar Es Salaa, imemkumbuka aliyhekuwa kocha wake wa wakati hueo Mmalawi Jack Chamangwana iliyefariki Dunia jumapili iliyopita. R.I.P Coach Jack Chamangwana. Ulikuwa sehemu ya mafanikio… Read More
  • Kitila Mkumbo atii agizo la Rais Magufuli Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo, ametekeleza kwa vitendo agizo alilopewa na Rais Magufuli, la kwenda kijijini Tundu, Wilayani Mikumi kushughulikia kero ya mradi wa maji kijijini hapo. Mei … Read More
  • Mzee Yussuf kulipua bomu   Aliyewahi kuwa mwimbaji mahiri wa muziki wa Taarab nchini ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarabu, Mzee Yusuph amefunguka na kusema kuwa hazitapita siku tatu lazima alipue bomu.  … Read More
  • TFF Yawapa Agizo Yanga la Kufanya Uchaguzi   Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeitaka klabu ya Yanga kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi za viongozi wake waliojiuzulu ikiwemo ya Mwenyekiti kwa wakati kwani tayari muda umeshapita.Agizo hilo limetolewa kwa M… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE