May 23, 2016

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema amesema kitendo cha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kumng'oa Waziri wa Mambo ya Ndani Charles Kitwanga kunatokana na Bunge kukosa hadhi kutokana na mambo ambayo huendelea ndani ya ukumbi huo wa Bunge.
Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ameyasema hayo wakati akizungumza na EATV hususu tuhuma za wabunge kunywa pombe wakati wa kazi.
''Bunge maalumu la katiba Bungeni kulikuwa na 'bar' zinauza pombe na idadi ya mawaziri na wabunge wanaokunywa pombe haijifichi ni .normal' na hii inatokana na Bunge kukosa hadhi''
''Hadhi aliyopioteza Waziri wa Mambo ya Ndani Charles Kitwanga imesababihwa na hadhi lililopoteza Bunge na wabunge na viongozi wake, siku hizi mambo yanafanyika ya ajabu polisi wanaingia ndani ya bunge wanapiga watu wanachania wanawake nguo, kanuni hazifuatwi, hivyo Kitwanga katumika tuu kwa namna ya kujiridhisha lakini kupuuzwa kwa maoni ya kambi ya upinzani ambayo yalieleza kuhusu Waziri Kitwanga kuhusika na Lugumi ndiko kulipaswa kumng'oa''-Amesema Lema.
Aidha Lema amebainisha kwamba wananchi pia wanapaswa kulumiwa kwa kitendo cha kuwachagua wabunge na kuwaacha tuu bila kuwafuatilia wanachokifanya Bungeni.
Kuhusu Bunge kutorushwa 'Live' Lema amesema kwamba inashangaza kuwaona wananchi wanakaa kimnya, viongozi wa dini na taasisi mbalimbali na kuwaachia upinzani pekee hali ambayo si nzuri kwa maendeleo ya taifa.

Related Posts:

  • DAZ MWALIMU, ADATA Habari kutoka kwa chanzo cha uhakika zinadai kuwa msanii wa zamani wa kundi Daz Nundaz na hitmaker wa ‘Figure Namba 8′ Daz Baba amechanganyikiwa kutokana na hivi karibuni kuonekana akifanya vitendo ambavyo havilingan… Read More
  • SERENGETI FIESTA ,MOROGORO NOMA SANAAAAAA   Mwana dada Rachel akonga nyoyo za mashabiki Moro.  Sehemu ya mashabiki wa tamasha la serengeti fiesta 2013 wakishangilia vilivyo usiku huu.  Kushoto ni Alnord Kayanda na kulia ni Mpoki wakiwa na… Read More
  • HUU NI UNYAMA AZALIA CHOONI NA KUUA KICHANGA KWELI dunia inakwenda ukingoni, mwanamke mmoja anayedaiwa kuwa ni mke wa mtu, amefanya kitendo cha kinyama baada ya kujifungua msalani na kukiua kichanga chake. Tukio hilo limetokea hivi karibuni maeneo ya Mazizini, … Read More
  • MFAHAMU DJ FETTY WA CLOUDS FM     Nikitaja majina ya Watangazaji na Madj’s ambao ni kipenzi cha mashabiki wengi wa muziki walioko kwenye chat kwa hapa nchini ni lazima utakutana na jina ‘Fetty’ hautalikosa katika ukurasa wowote wa b… Read More
  • TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 NOMA SAANA NDANI YA IRINGA USIKU HUU Anaitwa Shilole na Skwadi lake wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013       Pichani ni sehemu ya wakazi wa Mkoa Iringa na vitongoji vyake wakiw… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE