May 22, 2016

image 

Manchester United wanatarajia kumtangaza Jose Mourinho kuwa kocha wake mpya, BBC Sport imeripoti.
Inaaminika kuwa deal hiyo na raia huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 53 ilikubaliwa kabla ya ushindi wa United kwenye fainali ya kombe la FA dhidi ya Crystal Palace Jumamosi.
Ikiwa United imeshindwa kufuzu kushiriki kombe la mabingwa wa Ulaya chini ya kocha wake wa sasa, Louis van Gaal, uongozi wa Old Trafford unafikiriwa kuamua kufanya mabadiliko yanayohitajika.
Mourinho amekuwa benchi tangu atimuliwe na Chelsea December mwaka jana.
Klabu hiyo imepanga kutangaza ujio wake mapema wiki ijayo baada ya kumwambia Van Gaal, 64, afungashe virago vyake.
Kocha huyo raia wa Uholanzi bado ana msimu mmoja kwenye mkataba wake wa miaka mitatu na licha ya kutumia paundi milioni 250 kusajili wachezaji wapya, ukocha wake umewaangusha mashabiki wengi kwa timu yake kumaliza katika nafasi ya nne na kisha ya tano kwenye ligi kuu ya England katika misimu miwili aliyoifundisha.
Mourinho alikuwa kwenye mchezo wa masumbwi Jumamosi hii ambapo bondia David Haye alishinda lakini alikataa kuongea chochote iwapo anaenda kumrithi Van Gaal.
Mourinho ni mmoja wa makocha waliofanikiwa zaidi huku akishinda vikombe vitatu akiwa na Chelsea, pamoja na kuingoza  Porto na Inter Milan kwenye ushindi wa ligi ya mabingwa mwaka 2004 na 2010.
Aliwahi pia kuwa kocha wa Real Madrid na kuiwezesha kushinda kombe la Spanish La Liga mwaka 2012.

Related Posts:

  • Tumekuwekea hapa Magazeti ya leo hii upitie japo kwa ufupi tu Habari ndugu yetu mpendwa. Karibu katika magazeti yetu ya leo hii Ijumaa January 15 2016 upitie japo kwa ufupi tu kile kilichopewa kipaumbele leo hii. Share na mwenzio … Read More
  • Rais aondoa marufuku ya nyweleMarufuku hiyo ilikuwa imetolewa mapema mwezi huu Rais wa Gambia Yahya Jammeh ameondoa agizo la kuwataka wafanyakazi wa kike serikalini wawe wakijifunika nywele wakiwa kazini. Marufuku hiyo, iliyotolewa tarehe 4 Januari, … Read More
  • Tanzia: Celine Dion afiwa na mumewe Rene Angelil alihudumu kama meneja wa Celine Dion hadi 2014 Rene Angelil, mume wa mwanamuziki mashuhuri duniani Celine Dion, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 73, mwanamuziki huyo ametangaza. Bw Angelil, aliyemuoa Dion … Read More
  • Whatsapp na viber kudhibitiwaWhatasap ina watumiaji Zaidi ya milioni kumi nchini Afrika Kusini Mitandao ya whatsapp na viber huenda ikadhibitiwa Afrika Kusini ikitegemea matokeo ya vikao vya bunge baadaye mwezi huu, umeripoti mtandao unaoheshimika wa Fin… Read More
  • Baadhi ya wanaotumia Internet Explorer hatarini Inakadiriwa kwamba watu 340 milioni wanatumia matoleo hayo Microsoft imetangaza kwamba imeacha kutoa usaidizi wa kiufundi kwa matoleo ya awali ya kisakuzi chake cha Internet Explorer na kuwaweka hatarini mamilioni ya watu wan… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE