
Marekani ilisema wakati huo kwamba misaada mingine hatahivyo haitaathiriwa.
Haji Ssemboja profesa wa maswala ya kiuchumi alikiambia chombo cha habari cha Reuters kwamba usaidizi huo mpya unamaanisha kwamba Marekani inafurahishwa na mabadiliko yanayofanyika serikalini.
''Ijapokuwa mpango wa MCC na ufadhili huu ni mipango miwili tofauti ,msaada huu ni ishara kwamba Tanzania inaelekea katika njia nzuri'',alisema.
Ubalozi wa Marekani umesema kuwa fedha hizo zitatolewa mwaka huu ili kusaidia afya,kilimo,mali asili,usimamizi,elimu,kawi na uongozi wa kidemokrasia.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment