October 31, 2016

Tokeo la picha la thomas mashali 
 Bondia Thomas Mashali, ameuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira usiku wa kuamkia leo, baada ya kupigiwa kelele za mwizi kufuatia ugomvi uliozuka maeneo ya Kimara, jijini Dar es Salaam.
Bondia, Francis Miyeyusho aliyekuwa mwanafunzi wake, ameiambia East Africa Radio kuwa Mashali aliumizwa vibaya kichwani. Amesema Jumapili hadi saa tisa alasiri walikuwa pamoja kwenye kikao cha masuala ya masumbwi na alimuaga kuwa anaenda Kimara.

“Baadaye nikaja kusikia story kwamba kuna mtu kagombana naye pale wamemchenjia wameanza kumuitia kelele za mwizi mitaa ya Kimara huko kwahiyo wamemchangia raia, wamempiga,” amesimulia Miyeyusho.

Bondia huyo amesema kuwa Mashali alikuwa amenyoa rasta zake na kwamba huenda hiyo ni sababu wananchi wengi walishindwa kumtambua.


Kwa upande wa baba yake mzazi, Mzee Christopher Mashali, amesema alipata taarifa hizo usiku akiwa amelala kutoka kwa vijana wanaomfahamu. Vijana hao walimweleza kuwa mtoto wake amepigwa vibaya kiasi cha kupasuliwa kichwa na usiku huo kuwapigia simu wanae wengine waliopo Dar.

Anasema Mashali alifariki Muhimbili kutokana na kuwa amejeruhiwa mno ikiwa ni pamoja na kutolewa ubongo. Mzee Mashali anasema mara ya mwisho kuwasiliana na mwanae ilikuwa jana (Jumapili) mchana.

“Alinitumia meseji ambayo bado ninayo hapa akaniambia ‘baba nipo kwenye kikao, nikimaliza kikao nitakujibu baba’ ndio mara ya mwisho nimewasiliana naye,” ameeleza mzee huyo.

Amesema kinachoendelea sasa ni kupata ripoti ya polisi, kupewa ruhusa ya kuuchukua mwili wa marehemu tayari kwa mazishi.

Mashali aliyezaliwa mwaka 1980, ameacha watoto watano.

                         

Related Posts:

  • Kuhusu ajali ya ndege iliyopindika, kumbe Rubani alikuwa na matatizo ya kiakiliAjali ya ndege Viongozi wa mashtaka nchini Ujerumani wanasema kuwa wamepata ushahidi unaosema kwamba rubani wa ndege ya Ujerumani ilioanguka katika milima ya ALPS na kuwaua abiria 150 alikuwa amemficha mwajiri wake kuhusu ugo… Read More
  • Mtoto wa miaka 2 avunja rekodi Mtoto wa miaka 2 aweka rekodi India Amini usiamini mtoto mwenye umri wa miaka miwili ameweka rekodi ya taifa ya ulengaji shabaha kwa mishale nchini India.  Kulingana na vitabu vya kumbukumbu ya rekodi za taifa, Dolly S… Read More
  • Matumla afanya kweli Mohamed Matumla akijitahidi kumbana vyema mpinzani wake Bondia Mohamed Matumla amefanikiwa kutoka kimasomaso baada ya kumchapa kwa points bondia mwenzake kutoka nchini China Wang Xin Hua katika mpambano wa raundi 10 uli… Read More
  • Muswada tata kupeleka waandishi jela wapita Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bunge limepitisha muswada mchungu kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari baada ya kupitisha Muswada wa Takwimu wa Mwaka 2013, ambao pamoja na mambo mengine unataka mwandishi at… Read More
  • Pitio la Magazeti ya leo hii ijumaa march 27Leo ijumaa 27/3/2015 tunakupatia fursa ya kujua kile kilichoandikwa katika magazeti ya leo japo kwa Vichwa vya Habari. Kama ukitakaka habari zaidi pitia katika meza za magazeti zilizo karibu nawe … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE