Mhe. James Mbatia (MB) Vunjo, na Mwenyekiti Taifa NCCR. Ametaka zoezi la
uhakiki wa vyeti feki ni vyema likanzia kwa Rais na viongozi wengine.
Binafsi naunga Mkono hoja ya Mhe.Mbati kwa sababu mbili tu.
1.Kiongozi hutakiwa kuongoza kwa Mfano, tulitegemea akianza Rais,
watafuata na viongozi wengine wote, PM, VP, W. N/W, RC, DC, Wabunge hadi
Madiwani.
Aidha, kuna mazoezi mengi hapo awali yalianzishwa na Rais na viongozi
wengine Tuliona wakati wa kampani ya UKIMWI na Malaria No More, Tuliona
Utambulisho wa makazi, Tuliona kwenye BVR na NIDA.
Ikumbukwe kuwa, JPM alikuwa mastari wa mbele, kwa maana wa kwanza katika Zoezi la UHAKIKI WA SIRAHA Mkoa wa Dar.
2. Kuonyesha uhalali wa zoezi husika, kuwa kama zoezi likianza na
Viongozi mara nyingi huchukuliwa ni serious na ni zoezi halali lisilo la
kibaguzi kwa baadhi ya kada tu.
Kwani Mpaka sasa kuna baadhi ya Mawaziri inasemekana wanatumia majina fake, so uhalali wa zoezi hili upo wapi?
My Take:
Zoezi lianze kusafisha Nyumbani kwanza ( Baraza la Mawaziri & vigogo)
0 MAONI YAKO:
Post a Comment