October 06, 2016

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhIRYJIQfJrA9E7525HoKxkZuxPkJfkkLoA8fY4mHL1T_0fj6US2OcyDoqqOHUw2oci31VWyp7e8OeJ18WPgzp95Nfeg4L61jw4M0OGbKHDOdnkJ2untrdQRXEdqMXdXJVRiPgYlrvpcfQ/s2560/%25255BUNSET%25255D.jpg

Klabu ya Azam FC imemtambulisha Adbul Mohammed kuwa General Manager wa klabu hiyo ambapo mbali na utambulisho huo wameeleza lengo kuu la kumpa wadhifa huo ndani ya timu yao.

C.E.O wa Azam FC Saad Kawemba amesema lengo la kumwajiri Abdul kama General Manager ni kuhakikisha mabingwa hao wa kombe la Kagame wanapiga hatua mbele kwenye upande wa professionalism.


“Tunamtambulisha mwenu Abdul Mohammed, rasmi ni mwanafamilia wa Azam FC, anaingia moja kwa moja kwenye secretariat ya Azam FC lengo ni kuhakikisha klabu yetu inapiga hatua kwenda kwenye professionalism,” amesema Kawemba wakati akimtambulisha Abdul Mohamed.

“Atakuwa ni General Manager wa klabu yetu akishughullika na masuala ya kila siku yanayohusu klabu yetu. Tunamkaribisha kwetu kwa nia moja tukiamini uzoefu wake na weledi wake utatusaidia Azam FC kuondoka katika hatua tuliyopo kwenda hatua nyingine ya mbele zaidi.”

Abdul amesema atahakikisha muundo na muonekano wa Azam unabadilika na kuwa wa kiueledi.

“Nimekuja kwenye klabu ya Azam kwa ajili ya kufanyanao kazi kujaribu kuona tunaivusha au kubadilisha muonekano na muundo wa klabu kwenda kwenye hali ya weledi zaidi,” amesema mwandishi huyo wa zamani wa idhaa ya Kiswahili ya BBC.

“Azam ni klabu changa lakini ni miongoni mwa klabu kubwa Tanzania, tunataka kuwapa mashabiki wetu aina flani ya utofauti ambao hauwezi kupatikana kwenye vilabu vingine isipokuwa Azam.”

Related Posts:

  • NEW VIDEO: KIBOKO YANGU- MWANA FA ft ALLY KIBA Hii ni video mpya ya mkali Hamisi Corleone Mwinjuma aka Mwana FA ya Kiboko yangu ni moja kati ya ambazo zimekuwa zikisubiriwa kwa hamu na watu wengi. Video imetayarishwa na Director Kelvin Bosco wa … Read More
  • PAPA AWASILI UFILIPINO Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani,Mtakatifu Francis, amewasili nchini Ufilipino, nchi yenye Wakatoliki wengi zaidi barani Asia, huku ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa. Maelfu ya Wafilipino wamejipanga katika misur… Read More
  • MARKEL: TUTAWALINDA WAYAHUDI NA WAISLA,U UJERUMANI Kansela Angela Merkel   Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel ameahidi kuwalinda Wayahudi na Waislamu wanaoishi nchini Ujerumani dhidi ya ubaguzi. Amesema demokrasia ndiyo njia bora ya kupambana na machafuko yanayo… Read More
  • RONALDO DE LIMA KUREJEA DIMBANI Ronaldo de Lima anavyoonekana sasa. Mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa ya brazil Ronaldo Luís Nazário de Lima anatarajia kurejea tena dimbani. De lima ameahidi kupunguza… Read More
  • WATANZANIA WENGI WAFUNGWA HONG KONG Kasisi mmoja raia wa Australia amefichua na kuthibitisha kuwa kuna idadi kubwa ya wafungwa wenye asili ya Afrika katika magereza ya Hong Kong, wengi wao wakiwa ni kutoka Tanzania. Kasisi huyo John Wortherspoon ambaye … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE