Serikali ya Tanzania imekubali ombi la kuipatia Kenya madaktari 500 watakaoisaidia nchi hiyo kukabiliana na tatizo la uhaba wa madaktari katika vituo vyake vya tiba hasa baada ya kutokea kwa mgomo wa madaktari nchini humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli amekubali kutoa madaktari hao, baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe wa viongozi wa Wizara ya Afya kutoka Kenya uliotumwa na Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta.Kiongozi wa ujumbe huo ambaye ni Waziri wa Afya wa Kenya Dkt. Cleopa Mailu amemueleza Rais Magufuli kuwa, baada ya kutokea mgomo wa madaktari pamoja na uamuzi wa nchi hiyo kugatua madaraka katika sekta ya afya, imebainika kuwa nchi hiyo ina upungufu mkubwa wa madaktari ambao hauwezi kumalizwa kwa kutegemea madaktari wanaosomeshwa nchini humo na badala yake wanahitaji madaktari kutoka nje ya nchiWaziri Mailu aliyeongozana na Gavana wa Kisumu Jack Ranguma amesema Kenya ipo tayari kuwalipa stahili zote madaktari 500 watakaopewa na Serikali ya Tanzania ikiwa ni pamoja na mishahara na nyumba za kuishi.Kwa upande wake waziri wa Afya wa Tanzania, Ummy Mwalimu amesema Wizara yake ipo tayari kutoa madaktari hao haraka iwezekanavyo kwa kuwa Tanzania inao madaktari wengi wazuri ambao wamemaliza masomo na hawajapata ajira na wengine wamemaliza mikataba yao ya kazi na bado wana uwezo wa kufanya kazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli amekubali kutoa madaktari hao, baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe wa viongozi wa Wizara ya Afya kutoka Kenya uliotumwa na Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta.Kiongozi wa ujumbe huo ambaye ni Waziri wa Afya wa Kenya Dkt. Cleopa Mailu amemueleza Rais Magufuli kuwa, baada ya kutokea mgomo wa madaktari pamoja na uamuzi wa nchi hiyo kugatua madaraka katika sekta ya afya, imebainika kuwa nchi hiyo ina upungufu mkubwa wa madaktari ambao hauwezi kumalizwa kwa kutegemea madaktari wanaosomeshwa nchini humo na badala yake wanahitaji madaktari kutoka nje ya nchiWaziri Mailu aliyeongozana na Gavana wa Kisumu Jack Ranguma amesema Kenya ipo tayari kuwalipa stahili zote madaktari 500 watakaopewa na Serikali ya Tanzania ikiwa ni pamoja na mishahara na nyumba za kuishi.Kwa upande wake waziri wa Afya wa Tanzania, Ummy Mwalimu amesema Wizara yake ipo tayari kutoa madaktari hao haraka iwezekanavyo kwa kuwa Tanzania inao madaktari wengi wazuri ambao wamemaliza masomo na hawajapata ajira na wengine wamemaliza mikataba yao ya kazi na bado wana uwezo wa kufanya kazi.
“Kwa hiyo nitoe wito kwa madaktari wote Tanzania ambao hawapo katika utumishi wa umma, hawapo katika hospitali teule na ambao hawapo katika hospitali za mashirika yasiyo ya kiserikali wanaolipwa na Serikali, waombe nafasi hizi". alisema waziri Mwalimu
0 MAONI YAKO:
Post a Comment