March 23, 2013



      Mwigizaji mahiri wa Bongo Movies Vicent Kigosi maarufu kama Ray amewatoa hofu 
mashabiki wake kuhusu filamu yake ya ‘Sister Mary’ kuwa haijafungiwa japo kuna baadhi ya sehemu wameambiwa wazifanyie marekebisho na baadaye itakuja kutoka.



    Ray amekuwa akilalamikia wahakiki wa kazi za wasanii kutowatendea haki pale wanapowapelekea kazi ambazo zinawagusa wahakiki na kushindwa kuzitendea maamuzi yalio sahihi.

“Kuna udhaifu mkubwa katika kuhakiki kazi ya mwisho ya msanii kwa kuwa wanaohakiki mara nyingi hawapendi filamu inayowagusa na kuwakosoa,” amesema Ray.

 Sister Mary ilidaiwa kuwa inalidhalilisha kanisa katoliki na hivyo mapadre kutaka ipigwe marufuku

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE