June 20, 2013

Afande  Sele akiwa na Madee siu ya msiba wa Ngwea
   
   Msanii  wa  uziki wa Hip  Hop  toka  mkoani  Morogoro ambaye ndiye  mfalme wa  Rhymes  Tanzania  Afande  Sele, ameweka wazi  juu  ya  taarifa iliyoandikwa  na wikipedia kwamba aliwahi kuchukua tuzo ya kili music. 
    Kupitia katika page yake ya Facebook Afande amesema kwamba hajawahi kuchukua tuzo yoyote zaidi ya ile ya Mfalme wa  Rhymes, zaidi  Afande  anasema

  Ukisoma historia yangu kupitia WIKIPEDIA kamusi elezo huru, kuna sehemu wameandika kuwa nilishawahi kushinda tuzo za kili wakati si kweli zaidi katika historia yangu yote ya muziki hapa bongo nimeshawahi kushinda tuzo moja tu ya 'KING OF RHYMES' ambayo hata hivyo nilipata kwa kupitia nguvu ya umma tu kwa kuwa 'king of rhymes' ndio shindano pekee katika historia ya muziki wa bongo lililoandaliwa na kuamuliwa kupitia nguvu ya umma kiasi cha kuteka hisia za raia wa rika zote kama ilivyo kwa uchaguzi wa rais.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE