January 31, 2014



  Kufuatia kifo cha mtangazaji wa East Africa Radio, Keneth Kidago Lyanga, ona alichosema afande sele
   Wkt huo kituo cha radio(fm) moro kilikuwa kimoja tu nacho ni Ukweli fm kinachomilikiwa na kanisa katoliki jimbo la morogoro,kisanii nilikuwa mchanga sana nikifanya kaz chini ya kaka,rafiki na mwlmu wangu jose mbilinyi(Sugu),CD zilikuwa ni kitu adimu na chenye thamani sana kiasi kwamba nyimbo nilizokuwa nashirikishwa na sugu ktk albam zake nyingi hazikuwa zinapelekwa radioni kama'single'zilikuwa zinabaki ndani ya albam tu(kanda za casset) ili kusukuma mauzo kwa mashabiki,lkn kulikuwa na dj/mtangazaji mmoja tu ndani ya radio ukweli nyakat hizo aliyekuwa ananikubali sana kama msanii wa kwanza kutoka moro kwenda dar 'kibishi' na kufanya kazi bora kabisa nikiwa na msanii mkubwa na mkali aliyekuwa anatisha kwa nyakat zile 2 proud,mr 2 baadae sugu na leo ni mh sugu,huyu dj/mtangazaj alikuwa na kiu kubwa ya kuona mimi nasikika kwa mashabiki wa nyumbani moro kwa kila hali hivyo akawa anathubutu kucheza hewani pale redioni zile nyimbo nilizoshirikishwa na sugu kwa kutumia'Tape'kanda za kaseti'kilazima' na kweli watu walisikia nami nikasikika ikawa ndio mwanzo wa mimi kukubalika nyumbani na ugenini,yeye aliitwa keneth kidago lyanga maarufu kama brother'K',baadae alihamia triple A fm Arusha,nj na mwisho alikuwa est africa radio akitumikia vipind vya michezo zaid,nina taarifa za kuumiza sana moyo wangu juu ya mtu huyu,Keny????RiP ndg wa damu!,,,,


R. I. P Brother k. Tunalia, tutakusahau, lakini mchango wako ni mkubwa sana kwetu na kwa jamii kwa jumla, nafasi yako itabaki daima. Nakumbuka wakati upo Radio Ukweli nami nikianza harakati zangu za mziki, uliniahdi mengi na ulinisaidia sana kwa kiasi kikubwa mno. Hukuwa na Roho mbaya, ulinijenge na nakumbuka pia wasanii wengi walikufwata kwa ushauri. Nakumbuka mengi sna kwako. Tangulia tutaonana nawe muda si mrefu kwani imeandikwa mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke basi siku zake za kuishi wala siyo nyingi. Pumzika pema Brother K

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE