January 04, 2014

Jackie Cliff… mrembo wa haja niliyeanza kumfahamu kwenye video ya She Got A Gwan ya Ngwair. Ni msichana aliyeenda hewani na Mungu kampelea haswaa. Ukikutana naye huwezi kumwangalia mara moja ukaridhika, lazima ugeukE kumwangalia tena.
Nilipata bahati ya kumhoji mwezi September mwaka jana kwenye fashion show ya Ally Rehmtullah iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam na katika maongezi yetu kuhusu Ngwair na kazi yake kama mrembo wa video nikagundua kuwa, Jackie ni msichana mpiganaji asiyejali kitu.
Jackie The Boss Lady, ni msichana anayejulikana kwa kuishi maisha ya kifahari yakiwemo kuendesha magari ya gharama ambayo wengi yaliwapa maswali mengi, ni wapi anapata fedha hizo? Ni kweli fani ya urembo inalipa hivyo? Sijasahau pia kuwa aliyekuwa mume wake, ni miongoni mwa madon wa Dar na ambaye alifungwa kwa miaka kadhaa kwa shutuma zile zile za sembe. 
.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE