April 11, 2014

Beki Kelvin Yondani hajulikani alipo, uongozi haujui na hata benchi la ufundi halitaki kulizungumzia suala Lake. Kocha Msaidizi, Charles Boniface Mkwasa amesema hajui lolote kuhusiana na beki huyo na asingependa kuzungumzia.

“Sina taarifa yoyote kuhusiana na na Yondani,” alisema.

Lakini alipoulizwa bosi wake, Hans ven der Pluijm, naye alisema anachofanya ni kufanya wachezaji waliopo.

“Sasa nisingependa kumzungumzia Yondani, waliopo ndiyo ninafanya nao kazi na nguvu tunaelekeza katika mechi zilizobaki na tunataka kushinda zote,” alisema.

Viongozi wamekuwa wakikwepa kulizungumzia, lakini Yondani inaelezwa aliondoka mara tu baada ya mechi ya Mgambo ambayo Yanga ililala kwa mabao 2-1 mjini Tanga.

Rafiki wa karibu wa Yondani, amesema kwamba, beki huyo alikasirishwa na kuvishwa lawama alizoona hazikuwa na msingi, kwamba alihujumu kwa kuwa alisababisha penalty iliyozaa bao la pili.

“Unajua yeye ni beki, kosa linaweza kutokea na anaona anaonewa bila sababu za msingi na mbaya kuna baadhi ya viongozi wanaonekana kuungana na wale wasiojua mpira na kusisitiza alisababisha penalty kwa makusudi.

“Sasa hali hiyo imemuudhi na ukizingatia alicheza kwa nguvu sana, alijituma sana siku ile kwa kuwa anajua umuhimu wa ubingwa,” alisema rafiki yake huyo wa karibu bila ya kusema Yondani amejijimbia wapi.

Kabla ya kujiunga na Yanga, wakati huo akiwa Simba, Yondani alikimbilia kwao Mwanza na kujichimbia chanzo likiwa suala la lawama na kushutumiwa kuwa aliifungisha Simba makusudi.

Source:udakuspecially.com

Related Posts:

  • Hoteli yashambuliwa Tripoli    Watu wenye silaha wameshambulia hoteli moja maarufu kufikiwa na wageni kutoka nje katika mji mkuu wa Libya, Tripoli, na kuua walinzi watatu na watu wengine 12 kujeruhiwa. Watu kadha wenye silaha walivamia h… Read More
  • Wanajeshi wawaua waasi waliojisalimisha    Wakaazi wa kazkazini magharibi mwa Burundi wameiambia BBC kwamba walishuhudia wanajeshi wa serikali wakiwaua waasi waliojisalimisha.  Wanakijiji wa mkoa wa Cibitoke walisema kuwa takriban waasi 17 wal… Read More
  • CUF- Waandamana leo. Prof Lipumba akamatwa na polisi  Leo January 27 2015 Chama cha wananchi Cuf- kimefanya maandamano ya kumbukumbu ya mauaji ya 2011 Visiwani Zanziba. Lakini katika maadhimisho hayo yameingia dosari baada ya viongozi wa ngazi za juu wa Cuf kukatwa na p… Read More
  • Viboko washambulia wavuvi    Mtu mmoja amefariki dunia na wawili kujeruhiwa baada ya kuvamiwa na wanyama aina ya kiboko wilayani Butiama. WAKAZI wa kijiji cha Chimati wilayani Butiama mkoani Mara wamekubwa na hofu kubwa baada kuibuka… Read More
  • Hakuna wa kutembelea nyota yangu -Ray C    Mwanamuziki Ray C ambae alitamba miaka ya nyuma na ngoma kali kibao ikiwemo Na wewe milele,Sogea sogea na nyingine nyingi amefunguka na kusema kuwa kwa sasa hakuna mtu atakae weza kutembelea nyota yake katik… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE