Marehemu Geogre Tyson pichani hapa alikuwa yupo kijiji cha Chilonwa Chamwino kwenye utoaji wa madawati katika shule ya msingi Chaula iliyopo Dodoma. Baada ya kumaliza shughuli hii huku akiwa kama producer wa The Mboni Show mauti yalimkuta majira ya saa 12 jioni masaa 4 tu toka tuanze safari ya kurudi Dar es Salaam maeneo fulani hivi kama unataka kukaribia GAIRO mjini.
Katika gari hilo walikuwa watu 8 ila yeye
pekee ndio aliyepoteza mauti na wengine kupata majiraha mwilini pamoja
na dereva wa gari hilo. Kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa hapa
Morogoro katika hospital ya mkoa Morogoro, baadae asubuhi mwili utaanza
safari ya kurudi Dar es Salaam


PICHA ZA CHINI NI BAADA YA AJALI



Source: djchokamusic.com
0 MAONI YAKO:
Post a Comment