January 22, 2015

 
 Baraza la mawaziri la Jamaica, limeidhinisha mswada ambao unahalalisha watu kumiliki kiwango kidogo cha Marijuana.
Ina maana kwamba hii ni mara ya kwanza kwa jamii ya 'Warastafarian' wanaotumia Bangi kwa sababu za kidini kuweza kuivuta hadharani bila ya kupatikana na hatia.
Mswada huo,pia unatawezesha kuwepo halmashauri itakayokua ikitoa leseni za kupandwa , kuuzwa na kusambazwa kwa Marijuana kwa sababu za kimatibabu.
Lakini uvutaji wa Bangi katika maeneo ya umma haitaruhusiwa. Mswada huo huenda ukaidhinishwa na baraza la Senate wiki ijayo.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE