Msanii Omary Nyembo alimaarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka na kusema
kuwa watu wa uhamiaji duniani kote huwa hawatambui umaarufu wa mtu pindi
wanapogundua kuna kitu hakijaenda sawa,Ommy Dimpoz amefunguka hayo kapitia ukurasa wake wa
intrgram baada ya mwimbaji kutoka Marekani Chris Brown kuzuiliwa
kuingia Canada na kusababisha kusitishwa kwa show zake mbili ambazo
alitakiwa kuzifanya Canada ndani ya wiki hii.
Ommy Dimpoz ameonyesha ni jinsi gani watanzania na mashabiki wake
walilipokelea suala lake tofauti na kuonyesha kuwa watu wengi walimcheka
na kumchamba wakiamini kuwa yeye ni mtu maarufu hivyo asingeweza
kupatwa na suala hilo.
"Pole braza Kristofa, haya ni Mambo ya kawaida ila Mwenzio
nilivyozuiwa kuingia Nchini kwenu Basi nilivyorudi kwetu
nimechekwaaa,Nimechambwaa khaa,hawajuagi mambo ya Uhamiaji hawajali we
nani."
Wiki ya wapendanao msanii Ommy Dimpoz alirudishwa Tanzania baada ya
kuzuiwa kuingia Marekani kwa kukosa vibali vinavyomruhusu kuingia nchi
hiyo kufanya show.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment