Aliyewahi kuwa Meneja wa wasanii na mwanzilishi wa kundi la Tip Top Connection, Abdu Bonge amefariki dunia ghafla usiku wa kuamkia leo akiwa nyumbani kwake.
Akizungumza na EATV, mmoja wa wasanii aliye kundi la Tip Top Connection Madee, amesema kuwa bado hajafahamu chanzo cha kifo ila amefariki ghafla usiku huu akiwa nyumbani na msiba upo Manzese Tip Top
RIP Abdu Bonge
#Repost from @madeeali
Dah et nlisema Ata Abdul bonge siku yako aijulikali...dah Leo imejulikana..nsingekua mimi bila wewe...nlijivunia kua nawewe..nlijiamin popote pale..ww ndio baba wa mziki wangu...Asa nani atanielekeza nkikosea kuandika?nenda My Godfather...ntakuja.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment