
Mohammed Emwazi ,mtu ambaye
alibadilika na kuwa ''chinja chinja'' wa kundi la islamic state kwa jina
'jihad John' Mohammed Emwazi, alifurushwa kutoka nchini Tanzania kwa
kuwa mlevi na mtu anayetoa matusi.,afisa moja wa polisi ameiambia BBC.
Emwazi
anasema alitishiwa na kuhojiwa chini ya maagizo ya shirika la upelelezi
la Uingereza MI5 alipoenda nchini humo mwaka 2009.
Taarifa ya Mohammed Emwazi nchini Tanzania
Lakini BBC imeonyeshwa rekodi za kuzuiliwa kwake tangu alipokamatwa.Afisa huyo amesema kuwa Emwazi hakuruhusiwa kuingia nchini Tanzania kwa sababu alikuwa amezua mgogoro katika uwanja wa ndege na kuwa na tabia za mlevi.
Emwazi ambaye ana zaidi ya miaka 20 na ambaye anatoka magharibi mwa London ametambuliwa kama mtu aliyeziba uso katika kanda kadhaa za video ambapo mateka wamechinjwa.

Emwazi
Emwazi amesema kuwa alikuwa mwanafunzi ambaye alikuwa katika likizo ya
safari wakati aliposafiri na kuingia Afrika mashariki kupitia uwanja wa
ndege wa Dar-e-salaam kutoka nchini Uholanzi miaka sita iliopita.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment