April 25, 2015

Bunge la Afrika Kusini kusita ili kupambana na ubaguzi  
Bunge la Afrika Kusini litasimamisha shughuli zake wiki ijayo kwa ajili ya kuendesha mapambano ya kupinga ukatili dhidi ya wageni nchini humo. Ripoti iliyotolewa jana na bunge hilo imesema kuwa, wiki ijayo bunge hilo litasimamisha vikao vyake kwa lengo la kuwaruhusu wabunge kwenda katika maeneo bunge yao na kufikisha ujumbe kwa wananchi ili kukomesha ubaguzi dhidi ya wageni. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mpango huo uliopendekezwa na serikali utaweza kusaidia kupunguza wimbi la mashambulizi dhidi ya wageni waishio nchini Afrika Kusini. Mbali na mpango huo kutajwa kuwa utasaidia kupunguza wimbi la ubaguzi, unaelezwa kuwa utasaidia pia kudhamini usalama wa wageni nchini humo. Mashambulizi dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini yameongezeka katika wiki za hivi karibuni, kufuatia matamshi ya Mfalme wa kabila la Zulu, Goodwill Zwelithini, aliyoyatoa mwezi uliopita akiwataka wageni kuondoka nchini humo. Hadi sasa watu kadhaa wamekwishauawa na wengine wengi kujeruhiwa. Tayari Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amelaani vitendo hivyo na ameshakutana na shakhsia 50 wanaoongoza taasisi za wageni waishio nchini humo na kujadiliana nao njia za kumaliza tatizo hilo.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE