April 11, 2015

Raia wa Kenya waliokwama Yemen warejea nyumbani 
 Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya imetangaza kuwa, zoezi la kurejeshwa nyumbani raia wa nchi hiyo kutoka Yemen, litaendelea. Kwa mujibu wa wizara hiyo, hadi sasa serikali ya Nairobi imeshawarejesha nyumbani makumi ya raia wake kutoka Yemen, kutokana na kushadidi mashambulizi ya Saudia nchini humo. Imesema kuwa, hatua hiyo imekuja kufuatia ombi la Wakenya waishio nchini Yemen kuitaka serikali yao kusaidia kuwatoa nchini humo ili kuokoa maisha yao kutokana na mashambulizi mtawalia ya ndege za kijeshi za Saudi Arabia na waitifaki wake zikiwemo Marekani na Israel. Hii ni katika hali ambayo siku ya Alkhamisi Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri ilitangaza kuondolewa raia wake 1,150 nchini Yemen kutokana na usalama kuwa mdogo nchini humo. China ni nchi nyengine ambayo imeondoa wanadiplomasia wake nchini Yemen. Hadi sasa karibu watu 1000 wamekwishauawa tangu Saudia ilipoanzisha mashambulizi yake ya kichokozi tarehe 26 Machi mwaka huu dhidi ya wananchi wa nchi hiyo jirani ya Kiarabu. Wakati huo huo, malaki ya Wayemen jana walimiminika mabarabarani mjini Sana'a na mikoa mingine ya nchi hiyo kulaani jinai za Saudia katika kuwaua raia wasio na hatia na kubomoa miundombinu sambamba na kutangaza kuiunga mkono Harakati ya Answarullah iliyosimama kidete kuwakomboa wananchi wa Yemen.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE