May 25, 2015

 
  
Rais Dk. Jakaya Kikwete.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Anthony Peter Mavunde kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma, kuanzia leo, Jumatatu, Mei 25, 2015.
Aidha, Rais Kikwete amefanya uhamisho wa wakuu 10 wa Wilaya kwa nia ya kuongeza ufanisi katika uongozi wa Wilaya mbali mbali nchini.
Katika mabadiliko hayo, Rais Kikwete amemhamisha Luteni Edward Ole Lenga kutoka Wilaya ya Mkalama, Mkoa wa Singida kwenda kuwa mkuu wa wilaya mpya ya Kyerwa, Mkoa wa Kagera. Luteni Lenga anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Kanali Benedict Kulikela Kitenga ambaye alifariki dunia Aprili 20, mwaka huu, 2015.
Wakuu wengine wa wilaya ambao Rais Kikwete amewahamisha ni Elizabeth Chalamila Mkwasa kutoka Wilaya ya Dodoma kwenda Wilaya ya Mvomero, Mkoa wa Morogoro, Dkt. Jasmine Tisike kutoka Wilaya ya Mpwapwa kwenda Wilaya ya Dodoma, Agnes Elias Hokororo kutoka Wilaya ya Namtumbo, Mkoa wa Ruvuma kwenda Wilaya ya Tunduru, mkoani humo humo na Fadhili Nkurlu kutoka Wilaya ya Misenyi, Mkoa wa Kagera kwenda Wilaya ya Mkalama.
Wengine ambao wamehamishwa ni Chande Bakari Nalicho kutoka Wilaya ya Tunduru kwenda Wilaya ya Namtumbo, Festo Shem Kiswaga kutoka Wilaya ya Mvomero kwenda Misenyi, Darry Ibrahim Rwegasira kutoka Wilaya ya Karagwe, Mkoa wa Kagera kwenda Wilaya ya Biharamulo, mkoani humo humo, Elias Choro John Tarimo kutoka Wilaya ya Biharamulo kwenda Chunya, Mkoa wa Mbeya na Deodatus Lukas Kinawiro kutoka Wilaya ya Chunya kwenda Wilaya ya Karagwe, Mkoa wa Kagera.
Imetolewa na; Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu – Dar es Salaam. 25 Mei, 2015

Related Posts:

  • Meneja wa Diamond Sallam - SK azungumzia majukumu yake WCB na kluhusu kumchukua Mavoco   Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam Sharraf amezungumzia majukumu yake kwenye label ya WCB. Akiongea na mtangazaji Divine Kweka kwenye kipindi cha The Premier cha Kings FM ya Njombe, Sallam alisema yeye ni men… Read More
  • Master J awachana wasanii wa Hip Hop Mtayarishaji mkongwe wa muziki hapa Bongo, Master Jay amewajia juu wasanii wa Hip Hop bongo kwa kushindwa kutumia fursa zilizopo. Miaka ya hivi karibuni muziki wa Hip Hop nchini umeonekana haulipi huku baadhi ya wasa… Read More
  • Wanafunzi wa UDSM waanzisha mgomo  Wanafunzi wa chuo kikuu cha cha Dar es salaam (Udsm) mpaka sasa wamegoma wakiishinikiza bodi ya mikopo kutoa fedha kwa ajili ya kujikimu. Makamu wa Rais wa serikali ya wanafunzi, Shamila Mshengema amesema mgomo h… Read More
  • Alosto ya G Nako hii hapa Mwanamuziki kutoka katika kundi la WEUSI Kampuni, G. Nako, amekuletea wimbo wake mpya unaoitwa Alosto. Katika wimbo huo G. Nako amewashirikisha wasanii Niki wa Pili pamoja na Chin Bees na wimbo huo umefanyika katika stud… Read More
  • Zitto Kabwe amtolea uvivu Rais Magufuli  Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama cha ACT Wazalendo na kiongozi wa chama hicho Zitto Kabwe, amemtolea uvivu rais Magufuli na kuandika hiki katika AC yake ya Facebook "Rais Magufuli tunakuunga mkono kwa dhati kupa… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE