July 27, 2015

 

Chama cha TLP kimesema hakipo tayari kuungana na chama kingine chochote kile kwa makubaliano ya kumsimamisha mgombea mmoja badala yake kitasimamisha mgombea wake makini ambaye ataingia katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi ya urais.
Kauli hiyo imetolewa na naibu katibu mkuu wa chama cha TLP taifa Dominata Rwechungura wakati akiongea na wananchi wa kata ya Kishogo wilayani Bukoba ambapo amewataka watanzania kuendelea kuwa na imani na chama hicho huku akiwasisitiza wananchi kutowasikiliza wanasiasa wanaopanda kwenye majukwaa na kuwarubuni.
Rwechungura ametoa tahadhari kwa watanzania ili wasikubali kununuliwa kwa gharama nafuu na wanasiasa wanaopitisha pesa kwa wananchi ili waweze kuchaguliwa hali ambayo inaweza kusababisha kupata viongozi wabovu wasio na sifa ya kuliongoza taifa.
Katika hatua nyingine naibu katibu mkuu wa TLP Dominata Rwechungura amelaani vikali juu ya wanasiasa wanao jilimbikizia pesa za walipakodi ambazo zilitakiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi huku makamu mwenyekiti wa TLP taifa Bw. Joas Kayura akiwataka watanzania kutofanya makosa katika uchaguzi mkuu ujao kwa kutochagua viongozi wabovu badala yake wawe makini na kuchangua viongozi wazalendo wenye sifa za kuliongoza taifa kwa umakini

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE