July 02, 2015

 

Idadi ya watu waliokufa katika ajali iliyohusisha basi na treni katika eneo la KIBAONI wilaya ya KILOSA mkoani MOROGORO imeongezeka na kufikia WATANO baada ya dereva wa basi kufariki wakati akipatiwa matibabu Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa MOROGORO Kamishna Msaidizi MUSA MARAMBO amesema tukio hilo limetokea baada ya basi lenye namba za usajili T837 CTM lililokuwa likienda MOROGORO kukatiza na kugonga treni.watu 25 wamejeruhiwa katika ajali hiyo baada ya  gari walilokuwa wakisafiria kugonga treni yenye nambari za usajili 88U3 lililokuwa linatokea mkoani Dodoma kuelekea Morogoro.Mganga mkuu wa wilaya Kilosa  DENNIS NGAROMBA ameelezea hali za wawagonjwa kuwa zinatofautiana ila bado wanaendelea na matibabu lakini pia ameeleza kuwa wanakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo huduma ya umeme hali iliyofanya baadhi ya wagonjwa kuhamishwa hospitalini hapo

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE