October 21, 2015

Jonathan 
Kiongozi wa ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi wa Tanzania waliotoka Jumuiya ya Madola ametoa wito kwa watakaoshindwa uchaguzini Tanzania kukubali matokeo.
Goodluck Jonathan, ambaye mwenyewe alishindwa uchaguzini na upinzani amesema uchaguzi ni kama biashara.
“Kuna kushinda na kushindwa,” amenukuliwa na gazeti la The Citizen la Tanzania.
  
Amesema kukubali matokeo kutasaidia kuepusha mzozo wa kisiasa.
Kutokana na kupanda kwa joto la kisiasa nchini humo, Watanzania wengi wamekuwa wakifuatilia kwa karibu yanayoandikwa magazetini.
Mwandishi wa BBC Ruth Nesoba aliwapata wengi wakizingira vituo vya kuuzia magazeti Dar es Salaam kujipasha habari.
Jonathan, aliyeshindwa uchaguzini na Muhammadu Buhari mwezi Machi, alikubali matokeo upesi baada ya kushindwa na kupuuzilia mbali ushauri wa waliomtaka kupinga matokeo.

Related Posts:

  • WATANZANIA WANNE WAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA JOMO KENYATTA    Watanzania wanne (mwanaume mmoja na wanawake watatu) wamekamatwa na kilo 2.2 za heroin kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA). Watanzania hao waliingia nchini Kenya kupitia Namanga na w… Read More
  • BN: YANGA WAPATA AJALI MOROWachezaji na viongozi wa tinu ya Yanga, wamepata ajali maeneo ya Mikese nje ya manispaa ya Morogoro kufuatia Bas walilokuwa wakisafilia kupinduka. Katika ajaki hiyo hakuna majeruhi wala mtu kufariki. Chanzo cha ajali ni mabas… Read More
  • NAZIZI AFA KIMAPENZI NA PRODUCER WA KIBONGO...AACHANA NA MUME WAKE Hivi karibuni, mmoja wa waasisi wa hip hop nchini Kenya, Nazizi, alithibitisha kuwa ameachana ma mume wake kutoka Tanzania, Vinny, na wapo katika harakati za kupeana talaka Naziz na Vinny wana mtoto mmoja wa kiume. Msani… Read More
  • MTOTO ALIYEZALIWA GEST, AFARIKI DUNIA Yule mtoto wa kiume aliyezaliwa gesti huku mama yake  Bi.Mwanaidi Athumani akifanya ngono na mume mwingine amefariki dunia jana. Baada ya kupokea taarifa hizo Mwandishi wa habari hizi alifika hospital&nbs… Read More
  • PICHA/ KIJANA ALIYEKUFA KWA SIMU JANA Taarifa iloenea sehem tofauti za mji wa Zanzibar:- Kuna kijana anajulikana kwa jina la Ally mkazi wa Michenzani (Kiswandui)jirani na kwa bi mkubwa stadi umri wake miaka 22 amefariki ghafla maghribi ya JANA,taarif… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE