March 09, 2016

Majaliwa: Dola bilioni 80 zinahitajika ujenzi miundombinu EAC
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 80 zinahitajika katika kukamilisha ujenzi wa miundombinu kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Kassim Majaliwa amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati akifungua kikao cha tano cha Bunge la tatu la Jumuiya ya Afrika Mashariki kitakachofanyika kwa muda wa wiki mbili. Majaliwa amebainisha kuwa, nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), zinahitaji dola za Kimarekani bilioni 20 ili kufanikisha ujenzi wa barabara, pamoja na dola za Kimarekani bilioni 30 ili kukamilisha ujenzi na ukarabati wa reli. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameongeza kuwa, dola za Kimarekani bilioni 10 zinahitajika katika upanuzi wa bandari, na ujenzi wa bandari mpya, na dola za Kimarekani bilioni tano zinahitajika kwa ajili ya ufufuaji wa umeme na miradi mbalimbali ya kuzalishia nishati hiyo.
Kuhusu ujenzi wa reli ya viwango vya kimataifa Waziri Mkuu wa Tanzania amesema kuwa, ukarabati na upembuzi yakinifu kuhusu ujenzi wake umeshaanza kwa baadhi ya nchi. Aidha katika kikao cha ufunguzi wa Bunge la tatu la Afrika Mashariki hapo jana, Spika wa Bunge la EAC, Daniel Kidega, alimwapisha mjumbe mpya wa bunge hilo, Balozi Augustine Mahiga ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wa Tanzania.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE