
Nilitaka kujiua kwa sababu ya Rihanna
Mwanamuziki Chris
Brown amesema kuwa alitaka kujiua baada ya kumshambulia aliyekuwa
mpenziwe Rihanna kabla ya tuzo za Grammy mwaka 2009.
Katika
kipande kifupi cha makala yake ya 'Karibu katika maisha
yangu',mwanamuziki huyo wa mtindo wa R & B amesema kuwa uhusiano wao
ulikuwa kama ndoto lakini akajihisi kama hayawani.''Nilikuwa katika kilele cha dunia,nyimbo zangu zikiongoza,nikapendwa na wengi nchini Marekani kabla ya kuanguka hadi kuwa adui wa uma'',alisema.

Chris Brown na Rihanna
Brown alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela kufuata shambulio hilo.Kifungo hicho kilisitishwa mwaka jana baada ya jaji moja kusema kuwa nyota huyo amekamilisha mahitaji yake yote na kufunga kesi hiyo rasmi.

Rihanna
Makala hiyo inayowaonyesha Jennifer Lopez,Usher,Mike
Tyson,Jamie Fox na Rita Ora,Chris Brown anasema kuwa ''Nilihisi kama
nyota ,lakini nilijiharibia''.''Nilikuwa nikilala.Sikuweza kula,nilijihisi maarufu'',alikiri.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment