
Shirika la habari la Reuters linasema polisi walirusha mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya mamia ya wafuasi wa Bw Katumbi waliomfuata hati kwenye afisi ya mwendesha mashtaka mkuu.
Alipokuwa akihojiwa, wafuasi hao walikuwa wakiimba “rais!”.
Baadhi waliingia katika majengo hayo na mmoja wa walioshuhudia ameambia Reuters kwamba wanne walikamatwa.
Bw Katumbi ametanusha madai yaliyotolewa na waziri wa haki wiki iliyopita kwamba aliwaajiri mamluki, wakiwemo wanajeshi kutoka Marekani.
Wafuasi wake wanasema madai hayo yanalenga kuvuruga juhudi zake za kutaka kumrithi Rais Joseph Kabila.
Serikali imekanusha madai kwamba Katumbi anaandamwa kwa sababu za kisiasa.
Uchaguzi mkuu unafaa kufanyika baadaye mwaka huu.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment