
Mkongwe
wa Liverpool ambaye kwa sasa anakipiga LA Galaxy ya Marekani, Steven
Gerrard ameweka wazi kuwa atarejea timu yake ya zamani Liverpool mapema
zaidi baada ya kudumu kwa misimu miwili katika ligi Marekani.
Akiwa
katika kipindi cha maswali na majibu kutoka kwa mashabiki, Gerrard
amesema kuwa anafurahia maisha ya LA Galaxy lakini anaamini ipo siku
ataichezea Liverpool kwa mara nyingine.
“Nitakwenda
nyumbani, sitaki kuwa katika tetesi ambazo siyo sahihi, nina furaha na
sehemu niliyopo sasa lakini upo wakati nitaiwakilisha klabu ya
Liverpool,” alisea Gerrard.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment