Rais wa zamani wa Burundi Kanali Jean-Baptiste
Bagaza amefariki akitibiwa nchini Ubelgiji.
Kanali Bagaza amekuwa akitibiwa kwa muda
katika hospitali ya Sainte Elisabeth mjini Brussels.
"Imethibitishwa, rais wa zamani Jean Baptiste
Bagaza amefariki dunia akiwa nchini Ubelgiji,2
ameandika mshauri wa rais wa Burundi Willy
Nyamitwe kwenye Twitter.
"Alikuwa seneta maisha.”
Kanali Bagaza aliingia madarakani Novemba 1976
kupitia mapinduzi ya kijeshi.
Aliondolewa madarakani kupitia mapinduzi
mengine yaliyoongozwa na binamu wake Meja
Pierre Buyoya Septemba 1987.
MWILI WA VICTORY SENGE KUPOKELEWA LEO SHINYANGA MJINI, MAZISHI JUMATANO
BUSHUSHU
-
Mazishi ya marehemu Victory Emmanuel Senge yanatarajiwa kufanyika Jumatano,
Mei 6, 2026 Mjini Shinyanga, kufuatia kifo chake kilichotokea Jumamosi, Mei...
4 hours ago





0 MAONI YAKO:
Post a Comment