June 08, 2016

13394916_1169120956479247_963583199_n

Muongozaji wa video za Bongo ambaye anafanya vizuri Msafiri Shabani kutoka kampuni ya Kwetu Studio amesema changamoto kubwa wanayokutana nayo waongozaji wa hapa nchini ni location.

Akiongea na E-Newz ya EATV, Msafiri alisema ameanza kwenda kufanya video zake Afrika Kusini kutokana na uhakika na uharaka wa upatikanaji wa vitu kwaajili ya kazi zao kwakuwa kwa Tanzania inachukua muda mrefu wa kupata ruhusa ya kukamilisha kazi zao.





Msafiri Shabani
“Unakuta unaambiwa uandike barua, barua yenyewe inaweza ikaenda kujadiliwa mpaka wewe unakuja kupewa jibu tayari umeshaenda South Afrika umeshuti na tayari video umeshatoa. Hata katika location unakuta mtu mpaka akugeie gari ama nyumba mpaka muwe mnajuana wakati ukienda South chochote unachokitaka vipo vya kukodi ni wewe tu ukiwa na pesa,” alisema.
Pia Msafiri aliongezea kuwa sababu nyingine inayowafanya wakashuti video hizo nje ni kutokana na kuangalia wengine wanafanya nini ili nao waweze kushika nafasi nzuri katika soko la ushindani pia akidai kuwa inasaidia kupandisha thamani ya msanii kwakuwa anaonekana ana uwezo wa kutengeneza pesa kwaajili ya kufanya kazi zake.

Related Posts:

  • Chidi Benzi aikwepa miaka miwili jela   MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imemwachia huru mwanamuziki Rashid Makwilo 'Chid Benz' baada ya kulipa faini ya shilingi laki tisa sh:900,000/=.  Awali Chidi Benzi alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela… Read More
  • New Audio: Ally Kiba - Chekecha cheketua Baada ya kufanya poa ndani na nje ya Tanzania na wimbo wake wa mwana, Mwanamuziki Ally Kiba sasa amekuja na ngoma yake mpya kabisa inayoitwa Chekecha cheketua. … Read More
  • Mchinjaji wa IS 'Jihadi John' atambuliwa   Bwana huyo ambaye taswira yake akiwachinja mateka kwa kisu bila huruma ndiyo nembo ya wapiganaji hao sasa ametambuliwa kuwa anatokea Uingereza. Shirika la Habari la BBC limetambua kuwa jina lake kamili ni Moham… Read More
  • Waliomuiba Albino Pendo Wakamatwa Mwanza   Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo, amesema watu wote waliohusika ‘kuiba’ mtoto mwenye ulemavu wa ngozi (albino) Pendo Emmanuel (4) katika kijiji cha Ndami wilayani Kwimba, Mwanza, wamekamatwa. … Read More
  • Tp Mazembe yasajili watatu    Kikosi cha TP Mazembe cha Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo  Timu ya TP Mazembe ya Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo imewasajili wachezaji watatu wapya toka kwenye timu ya taifa ya Ivory Coast. Nyota … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE