Rapper wa muziki kutoka Bongo, Nay wa Mitego amepanga
kuachia wimbo wa kwanza kutoka kwa msanii wake chini ya lebo yake ya
‘Free Nation 966’.
Lebo hiyo ya Nay wa Mitego inamiliki wasanii watatu lakini kwa kuanza amepanga kuachia wimbo wa msanii wake aitwaye ‘Tiki’.
Akiongea kwenye kipindi cha Friday Night Live, kinachoruka kupitia EATV, Nay wa Mitego alisema lebo yake itakuwa na utofauti na lebo nyingine kutokana na yeye kuwa kuwa mfanyabiashara.
“Unajua mimi ni msanii wa kwanza kuanza kusimamia wasanii wenzangu, mpaka sasa nina wasanii watatu ambao wapo chini ya Free Nation, lakini kwa kuanza tutaanza na mmoja ambaye tushakamilisha naye kila kitu anaitwa Tiki,” alisema Nay.
“Nadhani Lebo yangu itakuwa na utofauti na Lebo nyingi sababu moja mimi ni mfanyabiashara hivyo hata msanii naye mleta lazima anaiingizie pesa huku akiwakonga mashabiki zake kwa muziki mzuri,” aliongeza.
Lebo hiyo ya Nay wa Mitego inamiliki wasanii watatu lakini kwa kuanza amepanga kuachia wimbo wa msanii wake aitwaye ‘Tiki’.
Akiongea kwenye kipindi cha Friday Night Live, kinachoruka kupitia EATV, Nay wa Mitego alisema lebo yake itakuwa na utofauti na lebo nyingine kutokana na yeye kuwa kuwa mfanyabiashara.
“Unajua mimi ni msanii wa kwanza kuanza kusimamia wasanii wenzangu, mpaka sasa nina wasanii watatu ambao wapo chini ya Free Nation, lakini kwa kuanza tutaanza na mmoja ambaye tushakamilisha naye kila kitu anaitwa Tiki,” alisema Nay.
“Nadhani Lebo yangu itakuwa na utofauti na Lebo nyingi sababu moja mimi ni mfanyabiashara hivyo hata msanii naye mleta lazima anaiingizie pesa huku akiwakonga mashabiki zake kwa muziki mzuri,” aliongeza.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment