July 11, 2016

103019708_theresa-may-news-large_trans++Y1vlWu6X4ClJ13DpyYGHanCugcTyzyB-SXuPVffSvBI



 Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron amesema kuwa Theresa May atakuwa waziri mkuu wa nchini hiyo baada ya yeye kuachia madaraka jumatano jioni.

Theresa May ambaye alikuwa akipigia chapuo nchi hiyo kutojiondoa ndani ya Muungano wa Ulaya atairithi mikoba ya Cameron baada ya yeye kutangaza kuwa ataachia wadhifa huo kufuatia nchi hiyo kupiga kura ya kujitoa katika Muungano wa Ulaya.
May amebakia yeye kutwaa nafasi hiyo baada ya mwanasiasa Andrea Leadsom kujiweka pembeni kwa madai kuwa Uingereza inataka kiongozi imara na anaamini kuwa May anaweza kazi hiyo.

0C34DB6F000005DC-0-image-a-7_1427648070005
Waziri Cameron atahudhuria mkutano wa mwisho wa baraza siku ya Jumanne na atajibu maswali siku ya Jumatano asubuhi na jioni atakabidhi barua yake ya kujiuzulu kwa Malkia.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE