September 12, 2016

Kikosi cha uokozi nchini Afrika Kusini, kimeendelea na shughuli za kuwaokoa wachimba madini waliokwama katika mgodi wa Langlaagte kwa siku kadhaa sasa.
Idara ya matukio yasiyotarajiwa nchini Afrika Kusini imesema kuwa, wafanyakazi wake wa operesheni za uokozi wanaendelea na juhudi za kuwatafuta wachimba madini haramu ambao tangu siku ya Jumatano iliyopita wamekwama katika njia za chini ya ardhi katika mgodi uliofungwa mjini Johannesburg.
Njia za chini ya ardhi katika mgodi wa madini
Idara hiyo imesema kuwa hadi sasa idadi ya wachimba migodi hao waliokwama bado haijafahamika. Hii ni katika hali ambayo hadi sasa waokoaji wamefanikiwa kuwaondoa watu wanne kutoka chini ya ardhi na tayari kuna khofu kwamba wachimba mgodi waliosalia wamekwishafariki dunia. Mgodi wa madini wa Langlaagte ni wa kwanza kugunduliwa mwaka 1886 mjini Johannesburg, hata hivyo imepita miaka kadhaa ukiwa umefungwa.
Mchimbaji wa dhahabu wakiwa chini ya miamba ya mawe
Maelfu ya wachimba migodi kinyume cha sheria wamekuwa wakipita njia za chini ya ardhi na mashimo yaliyowahi kuchimbwa dhahabu kwa lengo la kutafuta dhahabu kwenye mgodi huo.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE