October 20, 2016

 398914ac00000578-3853760-image-a-113_1476926071174

Donald Trump hayupo tayari kuyakubali matokeo ya urais wa Marekani – iwapo akishindwa of course.
Mgombea wa Urais wa Marekani wa chama cha Republican, Donald Trump akizungumza kwenye mdahalo wa tatu uliofanyika Jumatano
Katika mdahalo wa tatu na wa mwisho uliofanyika Jumatano hii, mgombea huyo kupitia chama cha Republican, amesema ana wasiwasi kura zitaibiwa. Amedai kuwa mpinzani wake, Hillary Clinton wa chama cha Democratic, hakutakiwa hata kuwania nafasi hiyo.


 


39896aad00000578-3853760-image-a-188_1476931149200-1  
 
 
 
 


Mgombea wa Urais wa Marekani wa chama cha Democratic, Hillary Clinton akizungumza kwenye mdahalo huo
Amedai kuwa kuna wapiga kura kibao watakaopiga kura ambao hawastahili kufanya hivyo na wamenunuliwa na Clinton. Alimuelezea mpinzani wake kama mtu mwenye hatia ya makosa mengi makubwa na hakupaswa kugombea Urais.
Alikuwa akielezea kuhusu kashfa ya barua pepe iliyomgubika Clinton, ambayo amekuwa akiitumia kila wakutanapo. Kwa kauli yake, Trump ameonesha dhahiri kuwa hatokubaliana na matokeo ya uchaguzi huo utakaofanyika Nov. 8.
3989417200000578-3853760-image-a-152_1476928675957
Kaka yake Barack Obama, Malik alikuwepo kwenye mdahalo huo kwa mwaliko wa Trump, mgombea anayemuunga mkono
Kwa upande wake Clinton alidai kuwa Trump ni bingwa wa kulalamika kutotendewa haki.
“Every time Donald thinks things are not going in his direction, he claims whatever it is, it is rigged against him,” alisema Clinton. “The FBI conducted a yearlong investigation into my emails that concluded there was no case. There was even a time when he didn’t get an Emmy for his TV program three years in a row, and he started tweeting that the Emmys were rigged,” aliongeza Clinton.
3989a45000000578-3853760-image-a-193_1476932062413
Trump akiongozana na mkewe Melania kuingia kwenye mdahalo huo
Hata hivyo mgombea mwenza wa Trump, Mike Pence alisema watakubaliana na matokeo ya aina yoyote. Na hata meneja wa kampeni wa Trump, Kellyanne Conway, aliiambia CNN watakubaliana na lolote.
Mwisho wa mdahalo huo, Clinton alisusa kumpa mkono mpinzani wake.
Kwa mujibu wa kura za maoni za CNN za watu waliotazama mdahalo huo, Clinton ameshinda kwa mara ya tatu kwa kupata 52% na Trump kupata 39%.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE