October 22, 2016

yusuph-manji

MWENYEKITI wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji ameahirisha mkutano wake na wanachama wa klabu hiyo uliotarajiwa kufanyika kesho Jumapili kufuatia kupokea barua ya zuio la mkutano huo kutoka kwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wanachama wawili wa klabu hiyo Juma Magoma na aliyewahi kuwa mwansheria wa klabu hiyo, Frank Chacha ndiyo walioiomba mahakama hiyo izuie mkutano huo uliopangwa kufanyika kwenye Makao Makuu ya klabu hiyo yaliyopo Jangwani jijini Dar.

Manji ametoa tamko hilo la kuahirisha kwa mkutano huo limetolewa leo kwenye makao makuu ya klabu hiyo na kudai kuwa hawezi kuingilia uhuru wa mahakama kwani anaamini suala hilo litaisha na atatangaza tarehe nyingine ya kufanyika kwa kwa mkutano huo mara baada ya taratibu zote za kimahakama kukamilika.

Aidha Manji amewataka wanachama wa klabu hiyo kuwa wavumilivu huku akiwaomba wanachama waliokuwa watokee mikoani kuacha kuja jijini Dar es Salaam hadi hapo atakapotangaza upya.


                     

Related Posts:

  • Top 40 ya Nyimbo kali Africa ipo hivi, Aje ya Ali Kiba yashika namba 3 All voting closes every Friday at 11:00am and re-opens on Saturdays at 11:00am. Thanks for your participation. Tune into the #AfricanTop40 every Saturday between 08:00-11:00am CAT on transafricaradio.net / taradio.mobi … Read More
  • Picha:Fiesta ilivyoifunika Kahama. Jumapili Muleba   Ikiwa ni wiki moja imepita tangu tamasha la Tigo Fieasta 2016 kuzinduliwa rasmi pale jijini Mwanza na mkali kutoka Nigeria Wizkid, sasa ni mchakamchaka. Siku ya jana ilikuwa zamu ya wakazi wa Kahama ambao wali enj… Read More
  • Pluijm: Samatta ni mfano wa kuigwa KIWANGO kinachoonyeshwa na mshambuliaji wa Genk ya Ubelgiji, Mtanzania, Mbwana Samatta, kimemkuna Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm na mwisho akafafanua kuhusiana na uwezekano wa siku moja staa huyo kucheza katika… Read More
  • JWTZ yatangaza kufanya usafi nchi nzima september 1 Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) leo linaanza shamrashamra za maandalizi kuelekea siku ya maadhimisho ya 52 ya majeshi inayotarajiwa kufanyika Septemba Mosi mwaka huu kwa kufanya usafi na upandaji miti katik… Read More
  • Mamba Anyakuwa Mtu Ziwani Buchosa. Mkazi wa Kijiji cha Kakobe, Kata ya Kazunzu katika Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema, Mkoa Mwanza, Juma Abdallah (30) anadaiwa kuliwa na mamba na mabaki ya mwili wake bado hayajapatikana. Ofisa Mte… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE